Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, October 17, 2011

JAMANI DUNIA IMEISHA HEBU MUONENI HUYU DUME JIKE ETI KAPIGWA KISA BWANA


SHOGA maarufu anayeishi Jangwani jijini Dar es Salaam, Ibrahim Mohamed ‘Anty Suzy’, (pichani)  amenusurika kuuawa kwa kucharangwa visu na mwanaume anayedaiwa alikuwa na uhusiano naye.

Akizungumza na makachero  wetu mwanzoni mwa wiki hii nyumbani kwake Jangwani,  shoga huyo alisema tukio hilo lilitokea Oktoba 1, mwaka huu.

Anty Suzy aliongeza kuwa, siku ya tukio alikuwa akitoka kwa shoga yake alikokwenda kukopa fedha za matumizi baada ya mwanaume huyo aliyedai alikuwa mumewe kumpora kila kitu na kumuachia chumba cheupe.

Aliongeza kuwa, jamaa huyo aliamua kumfanyizia baada ya kuweka wazi kwenye vyombo vya habari kwamba ameacha vitendo vya kishoga kufuatia kuumwa mara kwa mara.

Mwanaume huyo ambaye si riziki alizidi kudai kuwa, wakati akirejea nyumbani shoga mwenzake alimfahamisha kuwa, bwana’ke alikuwa akimsubiri na alipoingia ndani akashituka anavamiwa na kupewa kipigo.

“Alipoona napiga mayowe ya kuomba msaada alitoa kisu akanikata mkononi na shingoni, alipotokea mwenye nyumba na majirani aliniachia na kukimbia,” alisema shoga huyo.

Taarifa ya kesi hiyo imetolewa Kituo cha Polisi Msimbazi na kufunguliwa jalada namba MS/RB/10695/2011 SHAMBULIO.

No comments:

Post a Comment