Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, June 28, 2012

PICHA YA PILI YA NYUMBA ILIYOUNGUA MAKUMBUSHO JIONI YA LEO

BREAKING NEWSS ILIYOTUFIKIA: HII NDIO NYUMBA INAYOUNGUA MAKUMBUSHO,PICHA ZITAENDELEA KUWAJIA

EXCLUSIVE ANGALIA HAPA PICHA ZA : UZINDUZI FIESTA 2012

EXCLUSIVE:HII NDIO KAULI MBIU YA FIESTA 2012 NA LOGO YAKE

ANGALIA JINSI HISPANIA ALIVYOMTOA Portugal vs España

Azam Academy yaitoa jasho Azam FC, Kurudiana Jumamosi Asubuhi


Japokuwa wamefungwa 2-1 lakini timu ya Azam Academy wamewapelekesha vilivyo kaka zao Azam FC kwenye mchezo wa kujipima nguvu uliopigwa jana asubuhi, kwenye uwanja wa Azam, Chamazi.
Timu hizo zinajiandaa na mashindano, Academy wanajiandaa na mashindano ya Rollingstone 2012 yatakayofanyika nchini Burundi wakati Azam FC wao wanajiandaa na mashindano ya Kombe la Kagame yatakayofanyika Dar es Salaam mwezi ujao.
Academy walicheza kandanda safi muda wote wa mchezo na kuwapa wakati mgumu Azam FC kutokana na uwezo wa wachezaji hao.
Vijana hao walio chini ya miaka 20 ingawa wengi wao ni chini ya miaka 17 wamecheza mchezo  huo siku moja baada ya kuifunga timu ya Iringa United kutoka mkoani Iringa mabao 7-0.
Katika mchezo dhidi ya Azam FC ambao Academy walifungwa 2-1, Academy walikuwa  wa kwanza kupata bao la mapema katika dakika ya tano ya mchezo kupitia kwa Joseph Kamwaga aliyeachia shuti lililomshinda kipa Deogratias Munishi ‘Dida’ wa Azam FC. Kimwaga ambaye anaaminika kuwa ndiye winga mwenye kasi zaidi nchini kwa sasa ambeye pia anachezea timu ya taifa ya Under 20 alikuwa mwiba kwa mabeki wa Azam FC muda wote wa mchezo.
Goli hilo lilidumu hadi mapumziko huku timu hiyo ikiwanyanyasa kaka zao kwa kuwaonyesha uwezo wao imara uliojengeka kutokana na mazoezi bora wanayopata chini ya makocha wao Nagul Vivek na Iddi Cheche.
Azam FC walitafuta nafasi ya kushinda lakini timu hiyo iliyocheza kipindi cha kwanza ikiongozwa na Gaudence Mwaikimba haikuweza kubadilisha matokeo hayo.
Kipindi cha pili kilianza vizuri vijana walikuja kwa kasi na kuzuia mashambulizi ya kaka zao Azam FC, lakini dakika mbili za mwisho makosa ya benchi la ufundi la Academy ya kubadilisha timu yao ili kutoa nafasi kwa wachezaji zaidi kupata nafasi ya kucheza yalipelekea Azam FC kutumia nafasi hiyo kusawazisha goli na kuongeza goli la Ushindi.
Goli la kwanza kwa Azam FC liliwekwa wavuni na mshambuliaji George ‘Blackberry’ Odhiambo kwa shuti la pembeni na goli la ushindi lilifungwa na mshambuliaji Zahoro Pazi kwa shuti la mbali nje ya eneo la penati.
Timu hizi zitarudiana siku ya Jumamosi Asubuhi ambapo kambi zote mbili zimetamba kushinda mchezo huo.
Kabla ya hapo hapo kesho asubuhi Azam Academy itashuka kwenye uwanja wa JKT Ruvu kukwaana na JKT Ruvu.

SELEMAN MATOLA KOCHA MPYA AFRICAN LYON


Hatimaye leo mchana mchezaji wa zamani na nahodha wa klabu ya Simba Selemani Matola amejiunga rasmi na klabu ya African Lyon ya Dar es Salaam kama bosi wa benchi la ufundi.

Matola ambaye pia alikuwa ni kocha wa timu ya vijana ya Simba amejiunga na klabu hiyo ambayo kwenye msimu uliopita ilinusurika kushuka daraja.

Mchezaji huyo wa zamani wa Simba anaenda African Lyon kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na kocha aliyetimuliwa Jumanne Chale ambaye aliiongoza timu hiyo msimu uliopita.

VINARA WA LIGI KUU SIMBA NA AZAM KUPEWA ZAWADI ZAO KESHOKUTWA



MABINGWA; Kikosi cha Simba msimu uliopita, kutoka kulia Okwi, Kaseja, Kapombe, Maftah, Kazimoto, Chollo, Uhuru, Yondan, Boban, Mafisango (marehemu) na Sunzu. Wengine ni Dk Kapinga wakati kocha Milovan amechuchumaa mbele. 
WADHAMINI wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Kampuni ya Vodacom itakabidhi zawadi kwa washindi wa ligi hiyo keshokutwa kwenye hoteli ya Double Tree Hilton mjini Dar es Salaam.
Mfungaji bora, John Bocco atapokea kitita keshokutwa

Rihanna anusurika na moto jijini London






Kikosi cha zima moto jijini London, Uingereza, kimesema mwanadada Rihanna ni miongoni mwa watu 300 waliotolewa kwenye moto ulioubuka mapema asubuhi jana kwenye lift ya hoteli hiyo.
Mwanamuziki huyo mwenye miaka 24, alitweet habari hiyo kwa wafuasi wake milioni 21 kwa kuweka picha ya gari la zimamoto na maneno yasemayo: “Roamin da streets since 6am! Fyah in da telly.”
Kikosi hicho kilisema king’ora cha hatari kililia saa 6:22 a.m. na askari kumi wa zimamoto walifanya kazi ya kuuzima moto huo uliozuka kwenye ghorofa ya saba ya hoteli ya kifahari ya Corinthia. Hakuna ripoti za majeruhi kutokana na moto huo.
Rihanna yupo nchini Uingereza kwa zaidi ya wiki moja sasa ambako amekuwa akifanya show mbalimbali ikiwa pamoja na kuwapa support Jay-Z na Kanye West ambao wapo ziarani barani Ulaya iitwayo ‘Watch the Throne Tour’.
Rihanna, Jay-Z, David Guetta na Elton John watakuwa miongoni mwa watumbuizaji kwenye sherehe ndefu za “London 2012 Festival’, ambazo zimeandaliwa kote nchini Uingereza kwendana na michezo ya kiangazi ya olimpiki mwaka huu mjini London.
Sherehe hizo ambazo zimeanza, zitaendelea hadi Sept. 9, na kujumuisha matukio na performance 12,000.
Kutakuwepo na matukio mbalimbali katika masuala ya filamu, muziki, mitindo, sanaa za majukwaa, dance na sanaa za mikono.
Website ya mtandao huo imesema hizo ni sherehe kubwa kuwahi kufanyika nchini Uingereza zikiwa na bajeti ya takriban dola milioni 86.
                                            SOURCE BONGO 5

Mwinyi ajitoa machozi band


Aliyekuwa mwimbaji wa bendi ya Machozi inayomilikiwa na mwanadada Lady Jaydee amesema sababu za kujiondoa kwenye bendi hiyo ni kutokana na ubabaishaji mkubwa unaoendelea.
Akiongea na Clouds Fm jana, Mwinyi amesema hakufukuzwa kwenye bendi hiyo bali aliamua kuondoka mwenyewe baada ya kuchoshwa na ahadi za uongo kutoka kwa uongozi wa bendi hiyo.
Amesema kuwa kwa muda mrefu ameuvumilia ule aliouita ‘mkataba wa kijinga’ aliokuwa anautumikia kwa malipo ya kila mwisho wa wiki ambayo hata hivyo yalikuwa kiduchu na wakati mwingine alikuwa hakuti bahasha yake.
Mwinyi ambaye pia ni model, alieleza kuwa pamoja na bendi nyingi kutangaza nia ya kumchukua kwa ahadi za mkwanja mrefu, aliendelelea kuuvumilia ‘uswahili’ wa Machozi bendi na heshima yake kwa Lady Jaydee huku akiimba ‘for fun tu’.

Amesema Lady Jaydee alikuwa akimwonesha dharau kubwa na kujiona yuko juu wakati bendi yakeisingefika hapo ilipo bila ya mchango wake.
Mwimbaji huyo aliongeza kwa kusema kuwa sifa za nje za bendi hiyo ni kubwa lakini ukweli wa ndani ni kuwa haina lolote zaidi ya uswahili na ubabaishaji mwingi.
Mwinyi si msanii pekee aliyejitoa hivi karibuni kwenye bendi hiyo ya Machozi.
Mwimbaji mwingine aitwaye Sam ameamua kwenda kutafuta riziki kwenye bendi ya Skylight inayomilikiwa na mshiriki wa zamani wa Tusker Project Fame,Aneth Kushaba kwa mkataba wa mwaka mmoja wenye thamani ya shilingi milioni sita.
Clouds Fm walipojaribu kumpigia simu Gadner Habash kuelezea masuala hayo aliwapa jibu la ‘NO COMMENT’.

Bob Junior kufunga ndoa Billicanas July Mosi


Mwanamuziki na producer anayemiliki studio ya Sharobaro Records, Bob Junior aka Mr. Chocolate Flava, ameamua kufungua ndoa kwa style ya aina yake.
Amesema harusi yake itakayofanyika jumapili ya tarehe moja mwezi July mwaka huu, pamoja na kufanyika nyumbani itatinga ndani ya club ya Billicanas ambapo kila mtu anaruhusiwa kuhudhuria.
Rais huyo wa masharobaro amesema wiki hii atapanda boti hadi Zanzibar kwenda kumfuata ‘mwali’ ili aisaliti rasmi kambi maarufu ya makapela.
Bob Junior anayesifika kwa kukata ‘mauno’ kwenye video zake, amesema amechoka kuishi maisha ya ujana na sasa anahitaji kuwa na familia.
“Tunapiga show kila siku na kupata hela nyingi kwanini nisioe,” aliiambia 255 ya Clouds Fm jana.
Aliongeza kuwa dhumuni la kuamua kuoa ni kuepukana na vishawishi na maradhi kwakuwa watu maarufu kama yeye hujikuta wakitafutwa sana na wasichana.
.