Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, December 10, 2015

MeTL GROUP YASHEREKEA SIKU YA UHURU KWA KUFANYA USAFI COCO BEACH‏


IMG_7859
Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya MeTL Group, Bi. Fatema Dewji-Jaffer (kulia) akiongoza na Afisa Afya wa Manispaa ya Kinondoni, Bw. Kijumbe kuelekea kwenye eneo la usafi mara baada ya kuwasili kwenye fukwe za Coco Beach ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru wa Tanzania kama alivyoagiza Mhe Rais Dkt. John Pombe Magufuli, ambapo zoezi hilo limefanyika nchini kote Dec 9, 2015.
Na Rabi Hume, Modewjiblog
Kampuni ya Mohamed Enterprises Tanzania Limited (MeTL Group) imesherekea sherehe za Uhuru wa Tanganyika, Disemba 9 kwa kufanya usafi katika ufukwe wa Coco Beach kama jinsi alivyoagiza rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuagiza kuwa siku ya Uhuru itumike kufanya usafi kutokana na kushamiri kwa uchafu katika mazingira yanayotuzunguka.
Kwa kufata agizo hilo la Dkt. Magufuli, MeTL Group kwa kujumuisha viongozi wa kampuni na wafanyakazi wake imefanya usafi kwa pamoja katika ufukwe wa Coco Beach ili kusafisha eneo hilo ambalo linatumiwa na watu wa aina mbalimbali kwenda kujipumzisha pamoja ndugu na familia siku za mapumziko.
Hizi ni baadhi ya picha wakati wafanyakazi wa MeTL Group wakifanya usafi katika ufukwe wa Coco Beach;
IMG_7779
Baadhi ya wafanyakazi wa makampuni ya MeTL Group wakiwasili kwenye fukwe za Coco Beach kushiriki zoezi la usafi.
IMG_7812
#HapaKaziTu........Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya MeTL Group, Bi. Fatema Dewji-Jaffer (kulia) akisaidiana na Kiongozi Mahusiano ya Kazi wa MeTL Group, Subrina Gulamali Bhatti kubeba moja ya gogo lililokuwa linazagaa kwenye fukwe hizo.
 
IMG_7815
IMG_7820
Wafanyakazi wa makampuni ya MeTL Group wakiendelea na zoezi la usafi katika fukwe za Coco Beach ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru wa Tanzania kama alivyoagiza Mhe Rais Dkt. John Pombe Magufuli, ambapo zoezi hilo limefanyika nchini kote Dec 9, 2015.
IMG_7739
Zoezi la kukusanya takataka na kuchoma mifuko ya nailoni iliyokuwa imezagaa kwenye fukwe za Coco Beach likiendelea.
IMG_7733
IMG_7739
IMG_7765
Wengine wakiendelea kufyeka vichaka vya majani katika fukwe za Coco Beach.
IMG_7717
Zoezi likiendelea.
IMG_7704
Takataka zikiendelea kukusanywa na kuchomwa moto.
IMG_7746
Takataka zikikusanywa kwenye viroba.
IMG_7832
Zoezi likiendelea kwa ushirikiano wa hali ya juu.
IMG_7879
IMG_7881
#HapaKaziTu ndio maneno waliyokuwa wakisema wafanyakazi wa MeTL Group wakiendelea na zoezi la kusafisha fukwe za Coco Beach jijini Dar.
IMG_7809
IMG_7847
Baadhi ya wafanyakazi wa MeTL Group katika picha ya pamoja.
IMG_7662
Picha za kumbukumbu baada ya kazi zilipigwa.
IMG_7955
Mkuu kitengo cha Rasimali watu anayeshughulikia wafanyakazi wa ndani (Local) kampuni ya MeTL Group, Masuma Mushtak (waliosimama wa pili kushoto) katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Makao Makuu ya Ofisi za MeTL Group.
IMG_7964
IMG_7971

No comments:

Post a Comment