Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, December 8, 2015

RC KILIMANJARO ,AMOSI MAKALA AWASIFU WAANDAAJI WA BONANZA LA MADESHO DAY

Timu ya Ushrika wakijandaa kuvuta kamba katika bonanza la kumbukumbu ya Mwenyekiti wa kwanza wa klabu ya Moshi veterani Marehemu Madesho Moye. 
Timu za Maveterani wa KIA na Kitambi noma ya Arusha wakioneshana kazi katika kuvuta kamba.
Mashindano ya Mbio za mita 100 pia zilikuwa kivutio hapa ,Salvatory Mtanange akionesha uwezo wa kukimbia mita 100 ambapo alifanikiwa kushinda.

 
Mwamuzi maarufu wa mchezo wa kukimbiza kuku nchini akiingia uwanjani kwa ajili ya mchezo huo.
Kikosi cha timu ya Ushirika Veterani.
Kikosi cha wachezaji wa timu ya Kitambi noma.
Wachezaji wa timu ya Moshi eterani wakiongozwa na nahodha wao mpya aliyesajiliwa katika kipindi hiki cha dirisha dogo,Amosi Makala ambaye pia ni mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro wakinyoosha kabla ya kuanza mpambano.
Amosi Makala akijaribu kutaka kupita walinzi wa timu ya Ushirika Veterani.
Amosi Makala akijiandaa kupiga mpira wa adhabu .
Baadhi ya Mashabiki wa timu mbalimbali za maveterani zilizoshiriki Bonanza la kumbukumbu ya Mwanzilishi wa klabu ya Moshi Veterani,Marehemu Madesho Moye. 
Mshambiliaji wa klabu ya Ushirika Veterani Tumaini Masue akijaribu kutafuta njia za kutaka kumpita mlinzi wa timu ya Kitambi noma.
Masue akijaribu kuzuia mara baada ya kushindwa kupita .
Bonanza la Kumbukumbu ya Madesho lilienda sanjari na sherehe ya kupokea Kipaimara cha mtoto wake Qareen Madesho ambaye aliongozana na familia yake hadi katika viwanja vya Moshi Club ambako Bonanza hilo lilifanyika.
Mke wa Marehemu Madesho,Shufaa Madesho alikuwepo uwanjani hapo kufuatilia Bonanza hilo.
Mke wa Marehemu Madesho ,Shufaa Madesho akiwa  na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Amosi Makala ambaye pia alikuwa mgeni rasmi katika Bonanza hilo wakifuatilia mchezo.
Zawadi zikatolewa kwa mchezaji Cunbert Ngambira wa timu ya Maveterani wa KIA baada ya kushinda mbio za Mita 100 kwa wenye umri wa miaka 30-40.
Zawadi zikatolewa kwa mshindi wa mbio za Mita 100 Salatory Mtanange wa Moshi veterani kwa wakimbiaji wenye umri kati ya miaka 40 na 50.
Mshindi wa pili kwa upande wa mpira wa Miguu timu ya Ushirika Veterani ,wakakabidhiwa kikombe,nahodha wa timu hiyo Erick akapokea kwa niaba ya timu.
Washindi wa pili timu ya Maveterani ya Best Maridadi ,wakakabidhiwa kikombe ,kikapokelewa na Ismail .
Washindi wa kwanza kwa upande wa mpira wa miguu timu ya Maveteran wa njia panda ya Ulaya KIA,wakakabidhiwa kikombe na mgeni rasmi ,Amosi Makala.
KIA wakifurahia kikombe chao cha kwanza tangu kuanzishwa kwa timu hiyo.
Mgeni rasmi katika Bonanza hilo mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Amosi Makala akizungumza mara baada ya kukabidhi zawadi kwa washindi.
Mke wa Marehemu Madesho akizungumza katika Bonanza hilo.
Baadhi ya ndugu waliofika katika Bonanza hilo.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini (0755659929).

No comments:

Post a Comment