Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, December 2, 2015

UNYAMA WA KUTISHA: DEREVA ACHINJWA KIKATILI



Salum Masoud enzi za uhai wake. INASIKITISHA! Salum Masoud (35), mkazi wa Kijichi, Rufiji mkoani Pwani ambaye alikuwa dereva wa magari ya kubeba mizigo mkoani humo ameuawa kikatili kwa kuchinjwa na watu wasiojulikana na ifuatayo ni simulizi ya kusikitisha kutoka kwa dada wa marehemu aitwaye Hawa Masoud, mkazi wa Mbagala, Dar.
Akifuta machozi na kuzungumza kwa kwikwi na gazeti hili hivi karibuni, Hawa alisema mazingira ya tukio la kuchinjwa kwa ndugu yake yamejaa utata.

“Taarifa za kuuawa kwa kaka yetu zilitufikia Novemba 10, mwaka huu baada ya watu wasiojulikana kumpigia simu dada wa mke wa marehemu na kumtaarifu.

“Binafsi nilishtushwa sana. Ilikuwa vigumu kuamini. Lakini hatukuwa na budi kukubaliana na hali halisi, tukaamua 


kukusanyana na kwenda eneo la tukio kufahamu nini kilitokea mpaka Salum akauawa kikatili namna hiyo.

No comments:

Post a Comment