Salum Masoud enzi za uhai wake. INASIKITISHA! Salum Masoud (35), mkazi wa Kijichi, Rufiji mkoani Pwani ambaye alikuwa dereva wa magari ya kubeba mizigo mkoani humo ameuawa kikatili kwa kuchinjwa na watu wasiojulikana na ifuatayo ni simulizi ya kusikitisha kutoka kwa dada wa marehemu aitwaye Hawa Masoud, mkazi wa Mbagala, Dar.
Akifuta machozi na kuzungumza kwa kwikwi na gazeti hili hivi
karibuni, Hawa alisema mazingira ya tukio la kuchinjwa kwa ndugu yake
yamejaa utata.
“Taarifa za kuuawa kwa kaka yetu zilitufikia Novemba 10, mwaka huu
baada ya watu wasiojulikana kumpigia simu dada wa mke wa marehemu na
kumtaarifu.
“Binafsi
nilishtushwa sana. Ilikuwa vigumu kuamini. Lakini hatukuwa na budi
kukubaliana na hali halisi, tukaamua
kukusanyana na kwenda eneo la tukio kufahamu nini kilitokea mpaka Salum akauawa kikatili namna hiyo.
kukusanyana na kwenda eneo la tukio kufahamu nini kilitokea mpaka Salum akauawa kikatili namna hiyo.
No comments:
Post a Comment