Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, July 30, 2012

WANAFUNZI WAMPIGA MWALIMU KWA KUTOSHIRIKI MGOMO




picha hiyo hapo juu sio halisi

Na Gideon    Mwakanosya, Songea.

MWALIMU  mmoja  wa jinsia ya kike aliyefahamika kwa jina moja  la Kahimba  wa shule ya msingi  ya Kambarage  iliyopo    Kata ya  Msamala katika Halmashauri ya  Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma  amajeruhiwa vibaya  kwa kupigwa  sehemu mbalimbali za mwili  na kundi  linalodaijwa kuwa ni la wanafunzi wa shule hiyo ambao  wanadaiwa kuwa na hasira  baada  ya walimu wengi wa shule hiyo kutoonekana  eneo la shule kufuatia mgomo wa chama cha  Walimu  (CWT).

Akizungumuza na waandishi wa habari hizi Mjini Songea  mwalimu mkuu wa shule ya msingi  Kambarage  Adolfina Ndunguru alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo alidai kuwa  ni udhalilishaji  mkubwa kwa mwalimu kupigwa na wanafunzi.

Ndunguru alisema kuwa  yeye pamoja na walimu wenzake  hawakuweza kufika  kwenye eneo la shule kwa kuwa wao ni walimu ambao wamekubaliana kugoma  kutokana na Serikali  kushindwa kutimiza  ahadi yao wanayodai.

Alifafanunua kuwa  inadaiwa kundi la wanafunzi lilipomuona mwalimu  Kahimba kwenye  eneo la shule hiyo lilimvamia na kuanza kumpiga mawe sehemu  mbalimbali za mwili na baadaye  alifanikiwa kukimbia.

Kwa upande wa baadhi ya walimu  wa shule za msingi,Sekondari na Chuo cha Ualimu cha Songea kilichopo Manispaa ya Songea ambao wameomba majina yao yahifadhiwe walisema kuwa  mgomo  utaendelea mpaka Serikali itakapo ridhia kuwalipa madai yao hasa ikizingatiwa kuwa  wao wanafanyakazi katika mazingira magumu.

Waandishi wa habari walifanikiwa kutembelea baadhi ya shule  za Msingi na sekondari ambazo zilikuwa hazina walimu kabisa na kwamba wanafunzi wa shule hizo  wakiwa wamezagaa mitaani huku wakiinung`unikia Serikali kwa kuto watendea haki walimu wao ambao alikuwa wakiwaandaa wanafunzi katika Mitihani  ya kumaliza Elimu ya Msingi na sekondari.

Shule zilizotembelewa na waandishi wa habari ambazo hazikuwa na walimu kabisa  ni Shule  za Msingi za Matarawe, Mwembechai, Sabasaba, Mkombozi, Kawawa, Mfaranyaki, Majengo, Songea, Kambarage, Msamala na Majimaji na shule za sekondari za matarawe, Mfaranyaki, Shule ya wavulana Songea na Shule ya wasichana  songea.

Kwa upande wake mmoja  wa wanafunzi  wa shule ya msingi Majimaji Tamimu Ajali anayesoma darasa la tano ameiomba Serikali kuharakisha kutekeleza madai ya walimu  wanayodai kwani bila kufanya hivyo kunauwezekano mkubwa  wa kushuka kwa kiwango cha Elimu hasa  ikizingatiwa kuwa  wanafunzi wapo kwenye maandalizi ya kufanya mitihani.

Tamimu alisema kuwa  ni vyema serikali ikatambua umuhimu  wa mwalimu kwa kumuuongezea mshahara  sawa na taaluma  zingine muhimu kwa mfano. Wanajeshi, Madaktari,Wauguzi na wahudumu wa afya.

Afisa Elimu wa halmashauri ya Manispaa ya Songea  Fulgensi Mponji amethibitisha kuwepo kwa mgomo huo wa walimu  amabapo alisema Manispaa hiyo ina shule  72, Sekondari za Serikari 23, Shule za seskondari za binafsi 13 ambazo  idadi kubwa ya walimu  hawakuwepo kwenye maeneo yao ya kazi.

Alisema kuwa tayari ameshawaagiza walimu wakuu  wa shule za msingi na waratibu Elimu  kata wote kukutananao katika shule ya msingi Mfaranyaki  kwa lengo kuwakutanisha walimu ili kuzungumzia namna ya kutatua tatizo hilo.

Naye  Katibu wa chama cha walimu mkoa wa Ruvuma  Luya Ng`onyani alisema kuwa mgomo  huo ni halali na umezingatia sheria ya ajira na mahusiano kazini ya mwaka 2004 kifungu cha  80 (1) ambapo hatua ya kwanza CWT kwa niaba  ya wanachama tayari imetekeleza  kutangaza mgogoro wa siku 30 kwa kujaza fomu  CMA  No: 1.

No comments:

Post a Comment