Pages

Tuesday, November 29, 2011

SHAMBULIO ndani ya MGAHAWA wa LADY JAY DE


mgahawa wa Lady Jaydee kwa ndani ambapo spray hiyo ndipo ilipotupwa wakati watu wakiwa wengi
Gardner  habash, mume wa mwimbaji lady Jay d ametoa taarifa kuhusu mgahawa wao wa NYUMBANI LOUNGE kufanyiwa shambulizi na mtu ambae hajafahamika mpaka sasa, ambae lengo lake lilikua kuharibu biashara ijumaa ya weekend iliyokwisha jana.
amesema “ilikua ghafla sana ijumaa usiku kwenye saa 7 au 8, na aliyefanya hilo jambo baya alifanya kwa haraka sana ili watu wasimuone, bahati mbaya sana ilikua ni muda ambao watu wamekaa wanaenjoy muziki wa machozi band, tulisikia tu kuna harufu kali ndio watu wakasema itakua ni PAPER SPRAY, uzuri ni kwamba watu hawakuchachawa, tulifungua milango ambayo ni mikubwa watu wakatoka kirahisi na baada ya harufu kuondoka watu wakarudi na kuendelea kuenjoy” – GARDNER
Gardner Habash wa kwanza kushoto
Habash amesema ukiacha tu uharibifu wa biashara, kitendo kilichofanyika ni hatari pia kwa afya ya binadamu, alafu biashara kama hii utasema uiharibu leo lakini kuna watu waelewa na wanafaham imefanyika kwa makusudi kwa hiyo huwezi kuwaondoa watu sehemu wanayoipenda kwa sababu umetupa vitu vichafu.
mpaka sasa mtu aliyeitupa hiyo spray bado hajafahamika ila lengo lake limefahamika, kwamba ni kutaka kuraribu biashara.

No comments:

Post a Comment