Pages

Wednesday, December 14, 2011

Arsenal yatimiza miaka 125


Imeandikwa na Idd Seif
Klabu ya Arsenal ilianzishwa na kundi la wafanyakazi wa kiwanda kilichokua kikitengeneza silaha kilichojulikana kama Woolwich Arsenal Armament Factory walipoamua kuunda klabu ya mpira wa miguu mnamo mwaka 1886.
Klabu hiyo ikacheza chini ya jina ''Dial Square''.
Arsenal
nembo ya Arsenal
Mechi ya kwanza ya klabu hio ilichezwa tareh 11 mwezi Disemba, mwaka 1886. Mda mfupi baada ya hapo jina Royal Arsenal likabandikwa klabu hio na klabu ikaendelea kucheza mechi za kirafiki huku ikishiriki mashindano ya makombe kwa miaka kadhaa.
Mnamo mwaka 1891 klabu hio ikabadili hadhi yake na kua ya wachezaji wa kulipwa na kubadili jina kua Woolwich Arsenal, na hatimaye kujiunga na Ligi ya soka mnamo mwaka 1893. Mnamo mwaka 1913, klabu hio ikahamia uwanja wa Highbury kaskazini mwa jiji la London ikichezea katika daraja la pili. Baada ya vita vikuu vya kwanza vya Dunia Arsenal ilikubaliwa kwa kura katika Ligi ya daraja la kwanza lililopanuliwa, na tangu hapo hadi leo Arsenal wamesalia katika Ligi kuu.
Arsenal
Arsenal leo
Miaka ya neema ya 30 na Chapman.Herbert Chapman alianza kuifunza Arsenal mnamo mwaka 1925, na mnamo mwaka 1930 akaiongoza klabu hio hadi kushinda Kombe lao la kwanza kabisa. Na kati ya mwaka 1933 na 1935 klabu hio ilishinda Ligi mfululizo, rekodi iliyovunjwa na vilabu vinne tu vya daraja ya juu.
Kwa bahati mbaya Kocha huyo Chapman alifariki katikati ya msimu wa neema ambapo tayari alikua ameisha jipatia sifa ya stadi wa kufundisha soka.
Mrithi wake akawa George Allison aliyeendeleza mtindo wa kutawala soka kwa muongo mzima, akishinda Kombe la FA mnamo mwaka 1936 na ushindi mwingine mnamo mwaka 1938. Katika kipindi hiki Arsenal ilijivunia baadhi ya wachezaji mahiri, Alex James, Ted Drake, Cliff Bastin, David Jack, Eddie Hapgood na George Male ni majina ya baadhi ya wachezaji wazuri kuwahi kusakata gozi katika Ligi ya soka.
Tony Adams
Nahodha Tony Adams
Vita vya Dunia vya pili
Vita vikuu vya pili vya dunia viliiathiri Arsenal lakini Tom Whittaker alipoteuliwa kua kocha matokeo yakaimarika na ufanisi kupatikana. Arsenal ilishinda Ligi ya mwaka 1947/48 na 1952/53; vilevile ikashinda Kombe la FA la mwaka 1950 na kumaliza wa pili mnamo mwaka 1952. Miaka ya 60 haikua na mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kushindwa kwenye fainali mbili za kombe la FA la mwaka 1968 na 1969 . Wakati huu Arsenal ilikua na kocha mpya, Bertie Mee aliyeiwezesha kushinda Kombe lake lwa kwanza la Ulaya mnamo mwaka 1969/70, ilipoichabanga Anderlecht 4-3 katika mechi mbili za ugenini na nyumbani.
Mambo mazuri yalijitokeza msimu uliofuata. Timu ya Arsenal ikiwa na wachezaji waliokuja jijengea majina kama Charlie George, George Armstrong, Ray Kennedy pamoja na nahodha wa Frank McLintock, walishinda Ligi na Kombe la FA kwa mpigo'. Waliweza kuupata ushindi kwenye uwanja wa mahasimu wao wa White Hart Lane, kisha wakaizaba Liverpool baada ya kipindi cha ziada kushinda Kombe la FA kwenye uwanja Mkuu wa Wembley. Timu hio ilirudi uwanja wa Wembley kwa fainali tatu mfululizo chini ya Kocha Terry Neill mwishoni mwa muongo - kwa ushindi wa 3-2 dhidi ya Manchester United. Mechi hio ilipata uimaarufu kama fainali ya dakika tanol'. The Gunners pia waliweza kufikia fainali ya Kombe la mshindi la mwaka 1980, wakiwa na wachezaji kama Graham Rix, Frank Stapleton, Pat Rice, David O'Leary na Liam Brady, lakini wakapoteza fainali hiyo kupitia mikwaju ya matuta dhidi ya klabu ya Valencia.
George Graham
Mnamo mwaka 1986 George Graham, mmoja wa wachezaji wa Timu ya mwaka 1970 iliyoshinda vikombe viwili vya mwaka 1971 alichaguliwa kuwa meneja kutoka kwa Don Howe naye akaleta mafanikio zaidi. Aliiwezesha Arsenal kushinda Kombe lake la kwanza la Ligi la mwaka 1986/87, kwa kuichapa Liverpool 2-0 kwenye uwanja wao wa Anfield.
Ushindi mwingine ulifuata msimu wa mwaka 1990/91, klabu hio iliposifika kwa mabeki wake wanne, waliopoteza mechi moja msimu mzima.
Wilshere
Jack Wilshere
Makombe zaidi yalifuata. Mnamo mwaka 1992/93 Arsenal ikawa klabu ya kwanza kushinda makombe ya mashindano yote ya soka katika msimu mmoja. Klabu iliyosulubiwa ilikua Sheffield Wednesday mara zote. Msimu uliofuata ufanisi wa Graham uliendelea. Kipindi cha ufanisi katika michuano ya Ulaya uliomalizika kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Parma ya Italia katika fainali kwenye uwanja wa mjini Copenhagen. Bao la ushindi likitiwa kimyani na Alan Smith. Msimu uliofuata ilishindwa kutetea taji hilo ikishindwa nkatika fainali ya mwaka 1995 na Real Zaragoza. Wakati wa fainali hii Kocha George Graham alikua ameisha ondoka akifuatiwa na Bruce Rioch, ambayr aliiongoza Arsenal kwa msimu mmoja pekee akikumbukwa kwa kumsajili nyota wa klabu hio Dennis Bergkamp.
Wenger
Arsene Wenger
Enzi ya Arsène Wenger
Mnamo mwaka 1997/98, Arsenal ilimpata mwalimu mpya, Arsene Wenger na katika msimu wake wa kwanza kwenye uwanja wa Highbury, Arsenal ikafanikiwa kwa kuweka rekodi ya kushinda vikombe viwili Ligi na Kombe la FA. Hili lilimuzesha Mfaransa huyu kushinda zawadi ya mwaka ya Carling kama Meneja bora. Dennis Bergkamp pia alitangazwa kua mchezaji bora wa wandishi wa habari pamoja na mchezaji bora wa wachezaji wanaocheza soka ya kulipwa. Ukawa msimu mzuri kwa klabu uliomalizika kwa wachezaji wawili klabu hio Emmanuel Petit na Patrick Vieira kuiwakilisha klabu katika kikosi cha Ufaransa kilichoshinda Kombe la Dunia mwaka 1998.
Msimu wa mwaka 2000 Arsenal ilimaliza ya pili ikishinda medali za fedha ikishiriki fainali ya kombe la Uefa ambapo ilimaliza kwenye fainali ikishindwa katika fainali. Mwaka 2001 klabu hio ikaishia kwenye robo fainali ya michuano ya Ligi ya mabingwa UEFA ilipoondolewa na Valencia.
Msimu wa Mwaka 2001/2002 hata hivyo yakatokea mabadiliko na klabu hio kushinda mataji mawili kwa mpigo ilipoichapa Chelsea katika Kombe la FA na kumaliza Ligi kwa mechi 13 bila kupoteza na ushindi wa kuridhisha wa bao 1-0 dhidi ya mahasimu wao Manchester United kwenye uwanja wa Old Trafford. Hivyo Arsenal ikaendelea msimu mzima bila kupoteza kwenye uwanja wake kwa msimu. Kutokana na hilo Arsene Wenger akatajwa kama Meneja bora wa Barclaycard huku mcheza kiungo Robert Pires akishinda tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa wandishi wa habari.
Emirates
Ndani ya uwanja wa Emirates

Msimu uliofuata Arsenal ilikosea kosea kutetea taji lake ingawa Gunners ilijitokeza kua klabu ya kwanza ya England katika zaidi ya kipindi cha miaka 20 kutetea taji lake la FA kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Southampton kwenye uwanja wa Cardiff. Mwaka huo Thierry Henry akashinda tuzo ya wanfdishi wa habari na pia ya wacheza soka ya kulipwa katika mwaka uliomuomuezesha kujiunga na miamba ya wachezaji kama Dennis Bergkamp waliofunga mabao 100.
Msimu wa 2003/2004 Arsenal ikashinda tena Ligi kuu ya soka bila kushindwa msimu mzima ikimaliza pointi 11 mbeke ya Chelsea. Arsenal ilivunja rekodi kadhaa ikielekea ushindi wake wa mara ya 13 wa Ligi ya England. Msimu huo ndipo alipowasili kijana mdogo Cesc Fabregas mwezi January na hadi mwisho wa Msimu akawa ameisha vunja rekodi ya mchezaji mwenye umri mdogo kushiriki mechi nyingi akiwa mwenye umri wa miaka 16 na siku 177.
Henry
Thierry Henry
Kushindwa katika nusu fainali na kwenye kombe la FA dhidi ya Manchester United na katika robo fainali ya Ligi ya mabingwa na Chelsea yalikwamisha matumaini yote ya ushindi wa mataji matatu. Hata hivyo mafanikio ya kutopotea yaliendelea msimu uliofuata na mnamo mwezi Agosti 2004 Arsenal ikaipita rekodi ya Nottingham Forest kwa kipindi kirefu bila kupoteza katika Ligi ya England. The Gunners wakashinda vikombe 5 katika misimu minne kwa ushindi dhidi ya Manchester United kupitia mikwaju ya peneti katika Kombe la FA.
Msimu wa mwisho kwenye uwanja wa Highbury ulikua wa mwaka 2005/06 na katika sherehe za kuuaga uwanja huo Arsenal ilimaliza Ligi katika nafasi ya nnena Ligi ya mabingwa. Rekodi ya Arsenal kwa hivyo kwenye uwanja wake wa Highbury ukawa mzuri wa kusifika. Ilicheza mechi 2,010, ilishinda mechi 1,196, ikatoka sare 475, na kupoteza mara 339, ikafunga jumla ya mabao 4,038, ikifungwa mabao 1,955.
Muhimu katika safari ya klabu hio kufikia fainali ya Ligi ya mabingwa mjini Paris mwaka 2005/2006. Ni mechi 12 bila kupoteza, ikiwa ni pamoja na kuweka rekodi mpya ya mfululizo wa mechi bila kufungwa bao hata moja(mechi 10). Mafanikio haya yaliiweka klabu hii kwenye barabara ya kuonana uso kwa uso na Barcelona katika fainali ya Ligi ya mabingwa dhidi ya Barcelona mjini Paris kwenye uwanja wa Stade de France.
Lens
Jens Lehman
Licha ya kumpoteza golkipa wake, Jens Lehman baada ya dakika 18 za mchezo, Arsenal ilitangulia kupata bao kupitia beki wake Sol Campbell lakini katika kipindi cha pili Barcelona ikafunga mara mbili, mabao yaliyovunja mashabiki wa Arsenal waliofuatana na klabu yao.
Uwanja wa Emirates
Emirates
Uwanja wa Emirates
Cesc
Cesc Fabregas
Wakati klabu hio ikijiandalia shughuli ya kuhama kutoka uwanja wa Highbury kuelekea uwanja wa Emirates, nahodha na mfungaji bora Thierry Henry akathibitisha nia yake ya kuendelea kuichezea klabu na wakati huo huo akashiriki emchi iliyoisaidia Ufaransa kufuzu kushiriki fainali za Kombe la Dunia nchini Ujerumani mnamo mwaka 2006.
Mnamo mwezi Julai mwaka 2006 Arsenal ikahama kutoka uwanja wa Highbury, uwanja wake wa miaka 93, na kuhamia kwenye uwanja wake mpya. Klabu ya Ajax ikawa mpinzani katika mechi ya kumuaga mchezaji aliyesifika na kuichezea Arsenal akiweka rekodi hadi nyingine Dennis Bergkamp. Na katika mechi hi ambapo Bergkamp alishiriki mechi yake ya mwisho ikiwa ni mechi ya kwanza kabisa kwenye uwanja mpya wa Emirates.

No comments:

Post a Comment