Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, January 11, 2012

MESSI, GUARDIOLA, FERGUSON WALAMBA TUZO ZA FIFA - HUKU BARCA, MADRID NA MAN UNITED WAKIUNDA KIKOSI CHA DUNIA CHA MWAKA 2011.


Top prize: Argentina's Lionel Messi won the Ballon D'Or for the third year in a rowLionel Messi alitunukiwa tuzo ya FIFA Ballon d’O kwa mara ya tatu mfululizo.
Barcelona;s 24-year old Argentina striker aliwashinda mchezaji mwenzie wa Barcelona Xavi na mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo katika tuzo hiyo ya mchezaji bora wa mwaka.
Happy boy: Messi poses with his award and Colombian singer Shakira Shemejiiiiiiiii Shakira akimpongeza Lionel Messi.
Messi, man of the match katika champions league final mwaka 2011, pia alishinda kombe la La Liga, Spanish Supercopa, UEFA Super Cup na Kombe la klabu bingwa ya dunia mwaka uliopita.
Manager wa Manchester United Sir Alex Ferguson na Xavi wote walitoa maneno ya heshima kwa Messi.
Ferguson alisema Messi anaweza kuwekwa katika mizani ya magwiji wa soka duniani katika miaka mingi ijayo, hata kama bado ana miaka 24.
‘Maneno yamekuwa yakisemwa kila kuhusu kwamba wachezaji kama Pele kutoka katika zama za miaka ya 50 wangeweza kucheza katika kipindi hiki, jibu ni kwamba wachezaji wakubwa wanaweza kucheza katika kizazi chochote. Lionel Messi angeweza kucheza katika miaka ya 1950s na sasa pia, kama ilivyo kwa Di Stefano, Pele, Maradona, Cruyff kwa sababu wote ni wachezaji magwiji.” –Fergie

Past and present: Messi is congratulated by former winners Michel Platini and RonaldoMessi akipongezwa na washindi wa zamani wa tuzo hiyo Micheal Platini na Ronaldo De Lima,

Xavi nae alimuunga mkono Ferguson kwa kusema:” Lionel bado mdogo, ana miaka 24 tu na nafikiri atavunja rekodi zote zilizopo katika huu mchezo. Atakuja kuwa moja ya wachezaji wakubwa waliowahi kutokea katika mchezo huu wa mpira wa miguu.”
Mapema jioni ya jana Ferguson na Pep Guardiola walizawadia tuzo katika shrehe hizo.

Sir Alex and Sepp Blatter
Ferguson alizawadiwa FIFA Presidential award for services to football, na alikabidhiwa tuzo hiyo na raisi wa FIFA Sepp Blatter.

Top man: Barcelona's Pep Guardiola wins the FIFA World Coach of the Year award
Pep Guardiola alitajwa kama kocha bora wa Dunia in 2011 baaada ya kuiongoza Barcelona kushinda makombe matano

Boy from Brazil: Neymar picks up the FIFA Puskas award for best goal (below)
Neymar alishinda tuzo ya Puskas kwa kufunga bao bora la mwaka.
Pia jana kilitangazwa kikosi bora cha mwaka kwa mujibu wa FIFA huku kikosi hicho kikitaliwa na wachezaji wa Barcelona, Manchester United na Real Madrid pekee.

The good and the great: Wayne Rooney receives the FIFA/FIFPro World XI award from Brazilian legend PeleWAYNE ROONEY AKIKABIDHIWA TUZO YA KUWA MOJA YA WACHEZAJI WALIOUNDA KIKOSI CHA MWAKA

KIKOSI CHA FIFA CHA MWAKA
Iker Casillas (Real Madrid), Dani Alves (Barcelona), Gerard Pique (Barcelona), Sergio Ramos (Real Madrid), Nemanja Vidic (Man Utd), Andres Iniesta (Barcelona), Xabi Alonso (Real Madrid), Xavi (Barcelona), Lionel Messi (Barcelona), Cristiano Ronaldo (Real Madrid), Wayne Rooney (Man Utd).

No comments:

Post a Comment