Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Saturday, May 12, 2012

ANGALIA HAPA JINSI GARI LA TP MAZEMBE LILIVYOVAMIWA HUKO SUDAN.


.
Tabia ya timu za kisudani kuzipokea vibaya timu pinzani zinapoenda kucheza nchini kwao umeendelea, baada ya Simba sasa ni TP Mazembe ambao jana mashabiki wa klabu ya Al Merreikh ya Sudan wameufanyia fujo msafara wa klabu ya Tout Puissant Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) mjini Khartoum, wakidai na wao walipokewa vibaya na klabu hiyo mjini Lubumbashi wiki mbili zilizopita.
Mazembe yenye washambuliaji wawili Watanzania, Mbwana Ally Samatta na Thomas Emmanuel Ulimwengu ipo Khartoum kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Merreikh, hatua ya 16 Bora.
Katika vurugu hizo, basi walilokuwa wamepanda wachezaji wa Mazembe limevunjwa vioo ambapo  hali za wachezaji bado hazijajulikana na sasa mechi hiyo iliyopangwa kufanyika kwenye Uwanja wa Omdurman, hatima yake ipo mikononi mwa Shirikisho la Soka Afrika (CAF)- ambalo linatarajiwa kuchukua hatua muda mfupi ujao, kubwa zaidi ikitarajiwa kuifuta mashindanoni Merreikh na kuifungia, hivyo Mazembe kusonga mbele. (kwa mujibu wa shaffihdauda.com)
Simba ambayo nayo iko Sudan kwa ajili ya mechi yao ya jumapili nayo imekiri kufanyiwa vitimbi ikiwemo kuzimiwa taa za uwanja wakiwa mazoezini, kulazwa hosteli badala ya hotelini pamoja na fitina nyingine kibao.

.

.

.
Umeipenda Hii Story? Share na Washkaji:

No comments:

Post a Comment