Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, May 31, 2012

Rais wa zamani wa Liberia kwenda jela miaka 50


Charles Taylor, katika moja ya nyakati alizokuwa akifuatilia shauri lake
Rais wa zamani wa Liberia, Charles taylor, amehukumiwa kifungo cha miaka 50 jela baada ya kukutwa na hatia katika kesi iliyokuwa ikiendeshwa dhidi yake ya kuhusika na uhalifu wa kivita.
Mwezi uliopita, mtawala huyo wa zamani wa Liberia, alikutwa na hatia ya kuhusika katika kuviwezesha vikundi vya kigaidi nchini Sierra Leone, na mahakama maalum nchini Sierra Leone, kupitia kwa jaji wake mmoja imeeleza kuwa hukumu hiyo imeendana na kiwango cha makosa aliyoyatenda Bw. Taylor.
Taylor mwenyewe kwa upande wake ameendelea kusisitiza kuwa hakuhusika na tuhuma zilizopelekea kuhukumiwa kifungo hicho na taarifa za awali zinaeleza kuwa anatarajiwa kukata rufaa kupinga hukumu hiyo. Mchakato wa kukata rufaa hiyo unaweza kuchukua hadi miezi sita.
Alikuwepo mahakamani wakati hukumu dhidi yake ilipokuwa inasomwa, na hakuonekana kushtushwa na lolote lile zaidi ya kutulia mahali pake alipokuwa amekaa huku akiwa amevalia nadhifu kabisa suti yake na tai maridadi.
“Mtuhumiwa amekutwa na hatia ya kuhusika katika kuviwezesha vikundi vya kigaidi katika matukio mabaya kabisa ya kigaidi kuwahi kutokea katika historia ya dunia hii” alisikika jaji Richard Lussick akitamka wakati wa usomwaji wa hukumu hiyo ambayo imekuja baada ya miaka takriban mitano ya usikilizwaji wa shauri lenyewe.

No comments:

Post a Comment