Pages

Friday, June 29, 2012

BAN KI MOON AMUAGA RASMI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO



Ban Ki Moon akizungumza wakati wa hafla hiyo ambapo amempogeza na kushukurusu sana Migiro kwa namna alivyokuwa mshauri wake na mwalimu wake ambaye a anasema kwa  ualimu wake anampa alama ya plus plus plus. akatumia hafla hiyo kutangaza kwamba anamteua   Dkt. Asha- Rose Migiro kuwa mjumbe wake maalum katika  masuala ya ukimwi na ugonjwa wa ukimwi   Barani  Afrika. Migiro anaondoka  baada ya kuutumikia Umoja wa  Mataifa kwa miaka mitano na nusu.
Dkt. Asha-Rose Migiro akizungumza wakati wa hafla hiyo, akatoa shukrani zake kwa  Ban ki Moon kwa kumpatia heshima hiyo ya kihistoria ambayo haita kaa ifutike na kwamba  ameupokea uteuzi huo kwa mikoni miwili na hasa kutokana na kwamba tatizo la ugonjwa wa ukimwi ni tatizo ambalo analichukulia kwa uzito wa aina yake.na father kidevu

No comments:

Post a Comment