Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, June 14, 2012

Di Matteo sasa Meneja wa kudumu Chelsea


Roberto Di Matteo
Roberto Di Matteo
Chelsea hatimaye imemteua Roberto Di Matteo kama meneja wake wa kudumu kwa kutiliana saini mkataba wa miaka miwili.
ashinda FA na Ulaya
ashinda FA na Ulaya
Di Matteo aliwekwa kama kocha wa mda kufuatia kutimuliwa kwa Andre Villas-Boas mnamo mwezi Machi, na akaweza kuiongoza klabu hio akifanikiwa kuifikisha na kushinda fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya na vilevile kombe la FA la England.
Meneja huyo aliyekua kiongozi wa MK Dons na pia West Brom, Di Matteo alipoteza mechi tatu tu kati ya mechi 21 alizosimamia, na kutokana na hali hiyo wachezaji wengi wa klabu waliunga mkono ateuliwe kama meneja wa kudumu hususan baada ya kushinda kombe lililoikwepa klabu hio kwa mda mrefu la Mabingwa wa Ulaya

No comments:

Post a Comment