skip to main |
skip to sidebar
HUYU NDIO BABA ALIEKATA KICHWA CHA MWANAE KWA PANGA NA KWENDA NACHO POLISI.
Mwanaume mmoja mwenye umri wa
miaka 46 huko India amesema hajutii kumuua kwa kumkata kichwa mwanae wa
kike mwenye umri wa miaka 20 kutokana na mtoto huyo kuwa na uhusianoa wa
kimapenz na wanaume ambao baba yake alikua hawataki.
Mwanaume huyo aitwae Oghad
Singh amejisalimisha polisi akiwa ameshika kichwa cha mwanae na panga
alilotumia kukikata huku raia wa kijiji anachotoka wakishangaa.
Mwanaume huyo amesema alifanya
hicho kitendo pia kutokana na mwanae kuidhalilisha familia na huenda
ingepelekea dada zake wakakosa waume ambapo kama ilivyo desturi na mila
za wahindi mama mzazi na dada wanne wa marehemu hawakuruhusiwa
kuhudhuria mazishi yaliyotawaliwa na vilio na mshangao mkubwa.
Shirika la habari la AP
limeripoti kwamba Kitendo hicho cha kinyama alichokifanya huyo baba huyo
ni nadra sana kutokea kwenye nchi hiyo yenye watu zaidi ya bilioni 1.2.
Kama unapenda na watu wako
waisome hii habari unaweza kulike hapo chini sehemu ya facebook au
kutweet, naomba radhi kwa kuchelewa kuiweka kama nilivyoahidi mtu wangu
wa nguvu.
SOURCE MILLARD AYO
No comments:
Post a Comment