Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, July 30, 2012

MAMA TUNU PINDA AZINDUA MRADI WA MAJI KATIKA HOSPITALI YA MAWENZI LEO


Kampuni ya bia ya Serengeti Breweries Limited imetumia zaidi ya milioni 55 za kitanzania kujenga tanki kubwa la kuhifadhi maji kwa ajili ya matumizi ya hospitali ya Mawenzi mkoani Kilimanjaro.
Mradi huo umezinduliwa leo na mke wa waziri mkuu wa Jamhuri wa Muungano ya Tanzania Mama Tunu Pinda akiwa ndio mgeni rasmi katika uzinduzi huo ambapo katika kuuzindua mradi huo uliopata kuhudhuriwa na waandishi wa habari,maafisa kutoka ngazi mbalimbali serikalini mkoani hapo na wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro, mama Pinda alielezea kufurahishwa kwake na juhudi zinatofanywa na kampuni ya bia ya Serengeti katika kuisadia jamii ya watanzania bila kupendelea upande wowote.
“Mimi nashukuru sana kwamba leo nimepata fursa ya kusema yale niliyonayo moyoni kwa mda mrefu, kwamba kampuni hii ya bia ya Serengeti kwakweli mnafanya mambo makubwa ambayo hata serikali haikutegemea kama mtafanya, mmekua mstari wa mbele sana katika kuisaidia jamii inyowazunguka kwakujenga miradi mikubwa hasa yale yenye tija na na muhimu katika maisha ya kila siku kwa watanzania” aliseam mama Pinda huku akiwataka wakazi na watumiaji wa hospitali ya mawenzi mkoani Kilimanjaro na watanzania kwa ujumla kujenga imani na mahusiano mazuri na makampuni binafsi hasa yanayojali wateja wake na wananchi kwa ujumla kama kampuni ya bia Serengeti.

No comments:

Post a Comment