Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, August 10, 2012

UNATAKA KUMJUA ANAYEKUIBIA MUMEO?. MBINU HIZI ZITAKUFAA





UNATAKA KUMJUA ANAYEKUIBIA MUMEO?. MBINU HIZI ZITAKUFAA!. |
Ikague simu yake
Katika mazingira ya kawaida, haishauriwi kuikaguakagua simu ya mumeo kwani kufanya hivyo ni kuonesha jinsi usivyomuamini lakini unapohisi unaibiwa na hujui ni nani mwizi wako, unaweza kuanza kuikagua simu ya mpenzi wako kwa siri sana. Angalia simu zilizoingia na kutoka, meseji zilizotumwa na kuingia. Kama kuna mtu ambaye ana uhusiano naye, utagundua lakini tambua kwamba ni zoezi la muda mrefu na fanya hivyo bila mpenzi wako kugundua. Tumia muda anaokwenda kuoga, chooni na anapoisahau simu nyumbani, ipo siku utabaini siri nzito.
.
Ingia kwenye Facebook yake
Kama mumeo ni mtu wa facebook na unajua password yake, ingia mara kwa mara kwenye ukurasa wake. Kama ulikuwa hujui mtandao huo wa kijamii sasa hivi unatumiwa na wengi katika kuzisaliti ndoa zao. Waume za watu wanatumia njia hiyo kuwasiliana na vimada baada ya kubaini wakitumia simu ni rahisi kukamatwa. Kwa maana hiyo, tumia mbinu ya ushawishi kupata password yake na huko unaweza kumbaini mtu anayekuharibia.

3. Mfanyie sapraizikazini
Kama mumeo anafanya kazi, elewa kwamba wengi hutumia muda wa  kuwa na wapenzi wao wa pembeni. Unaweza kumuibukia siku mojamoja kazini kwake au kwenda sehemu ambayo hupendelea kula chakula cha mchana.
Kwa mfano siku ya kwanza umemkuta yuko na demu, ukaondoka kisha siku nyingine ukawakuta tena pamoja, ukaondoka na siku nyingine tena ukawaona katika mazingira hayo, akili yako itakupa jibu. Hata hivyo, katika njia hii uwe makini kwani inawezekana huyo msichana ni mfanyakazi mwenzake ambaye hupendelea kwenda naye lunch tu na hakuna kingine cha zaidi

4. Chunguza nguo zake unapozifua
Wakati unafua nguo zake, tumia muda mwingi kuzichunguza. Angalia kwenye waleti yake, unaweza kukutana na risiti zinazoonesha amenunua vitu vya kike ambavyo wewe hujaviona. Pia unaweza kukutana na vikaratasi vyenye namba za simu ambazo ukizipiga ni za mwanamke na ukimwambia wewe ni mke wa fulani, anakupa majibu ya kiwiziwizi. Pia kwenye nguo zake unaweza kubaini  nyekundu wakati wewe hutumii hiyo.

5. Muazime gari lake
Kama mpenzi wako analo gari, mshitukize kisha muombe gari lake uende sehemu. Kwa kumshitukiza atakuwa hajapata nafasi ya kulisafisha hivyo ukiwa nalo lichunguze kila sehemu. Unaweza kukutana na risiti, namba za simu au nguo na vitu vya kike ambavyo huvijui. Wapo ambao waliwahi kufanya hivyo na wamefanikiwa kubaini usaliti wanaofanyiwa.

6. Mshitukize baa
Yawezekana mumeo ni mnywaji wa pombe na umekuwa ukimpa uhuru wa kufanya hivyo bila kumfuatilia. Kama umebaini unasalitiwa na humjui anayekuibia penzi lako, siku moja muulize anakunywa pombe wapi, kwa kuwa amezoea huna tabia ya kumfuatilia, atakujibu. Siku hiyo mfuate, mwanamke utakayemkuta naye mnoti kisha ondoka bila mpenzi wako kujua. Siku nyingine, mbabatize tena akiwa baa na kama utamkuta na msichana yuleyule, basi mwekee alama na kwa uchunguzi ambao utaendelea nao, kuna siku utajua ukweli.

7. Mfuatilie
Hili nalo halishauriwi kulifanya kwani mpenzi wako akijua unamfuatilia, anaweza kukuacha kwani atajua humuamini na wengi hawapendi kuendelea kuishi na watu ambao hawawaamini. Ila sasa, ukishahisi unasalitiwa huna budi kufanya hivyo. Tumia watu kufuatilia nyendo zake kila anapokwenda na haitachukua siku nyingi utajua huyo mpenzi wako anakusaliti na mtu gani.
Kwa kifupi ni kwamba, unastahili kuwa na mtu muaminifu, anayekujali na kukupenda kwa dhati. Unapohisi mumeo si muaminifu, usikimbilie kuomba talaka au kuja juu kama moto wa kifuu bila kuwa na ushahidi. Tumia mbinu hizo hapo juu kutafuta ushahidi wa kile unachokihisi na mwishowe utafanya uamuzi sahihi

No comments:

Post a Comment