Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Saturday, January 12, 2013

MAANDALIZI YA SHEREHE ZA MAPINDUZI ZANZIBAR YAKAMILIKA



 Kamanda wa Brigedia nyuki Brigedia General Sharif Sheikh, akiwa pamoja na Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif, wakifurahia mwenendo mzima wa matayarisho ya gwaride  la Vikosi vya Ulinzi yaliyokuwa yakifanyika katika uwanja wa amani MJINI Zanzibar.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya Taifa ya sherehe na mapambo Balozi seif, akiwa na Waziri wake Kulia Mh. Mohd Aboud Mohd na Kamanda wa Brigedia Nyuki Brigedia General Shjarif Sheikh wakiangalia matayarisho ya mkwisho ya gwaride la sherehe za mapinduzi katika uwanja wa amani Mjini Zanzibar.
 'Watoto wa Kazi' Kikosi Maalum cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania { JWTZ }, Kikionyesha umahiri wake ndani ya Uwanja wa amani wakijiandaa na sherehe za maapinduzi zinazofanyika kesho Jumamosi Tarehe 12 Januri 2013, katika uwanja huo.
 Msanii wa Kikundi cha Utamaduni cha Hiari ya Moyo kutoka Mkoani Domoma kikipasha moto kujiandaa na utoaji burdani kwenye sherehe za maaadhimisho ya kutimia miaka 49 ya mapinduzi ya Zanzibar zitakazofikia kilele chake januari 12 2013.
 Kikundi cha Utamaduni ya mchanga mdogo kisiwani Pemba kikitoa burdani ya ngoma ya msewe katika matayarisho ya maadhimisho ya sherehe za kutimia Mikaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar hapo Uwanja wa Amani.

No comments:

Post a Comment