Pages

Monday, March 11, 2013

Nchimbi atimua mabosi sita polisi, makuruta 95



Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi amewafukuza kazi maofisa watano wa Polisi na kumsimamisha kazi kwa mwezi mmoja Kamishna msaidizi Mwandamizi wa jeshi hilo kutokana na makosa mbalimbali.
Pia, Dk Nchimbi amewafukuza makuruta 95 waliokuwa Chuo Cha Polisi (CCP), Moshi kutokana na kugundulika kutumia rushwa kupata ajira.
Kamishna msaidizi Mwandamizi wa Polisi aliyesimamishwa kwa mwezi mmoja ni Renatus Chalamila akihusishwa na rushwa katika kuajiri.
Alisema taarifa za uchunguzi za kamishna huyo, ambaye anashughulikia masuala ya ajira zimewasilishwa kwa Rais Jakaya Kikwete, ambaye ndiye mwenye mamlaka ya kumfukuza kazi.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Dk Nchimbi alisema maofisa watatu kati ya hao watano wamefukuzwa kutokana na kugundulika kuwa walikamata dawa za kulevya aina ya cocaine lakini zilipopelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali alidai zilikuwa ni chumvi na sukari.

No comments:

Post a Comment