Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Sunday, March 17, 2013

WALIOMTEKA NA KUMSULUBISHA KIBANDA HADHARANI




Hatimaye sakata la kutekwa, kuteswa na kujeruhiwa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, (TEF), Absalom Kibanda, limepata mwanga na watuhumiwa wa kadhia hiyo wataanikwa hadharani kesho.

Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, amesema timu iliyoundwa kuchunguza kutekwa, kuteswa na kujeruhiwa kwa Kibanda, itatoa taarifa kamili na idadi ya watu waliowakamata kuhusiana na tukio hilo.

Wakati Kova akieleza hilo, mitandao ya kijamii jana ilieleza kuhusu taarifa za kukamatwa kwa mtu aliyejulikana kwa jina la Ludovick Joseph kwa tuhuma za kuhusika kuteswa kwa Kibanda.

Kova alipoulizwa kuhusiana na taarifa hizo, aliomba apewe muda ili awasiliane na mwenyekiti wa timu iliyoundwa kuchunguza tukio hilo.

“Tangu asubuhi nilikuwa Mabwepande, ndiyo nimerudi ofisini muda sio mrefu, kuhusu hilo nimelisikia kupitia kwa waandishi wenzako walionipigia simu, nipe muda nilifuatilie,” alisema.

Baada ya kupigiwa tena, Kova alisema kwa mujibu wa maelekezo aliyopewa na timu hiyo, haikuwa muda muafaka kulizungumzia suala hilo jana.

No comments:

Post a Comment