Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, August 7, 2013

POLISI WAKAMATA MIFUKO 1312 YA SUKARI ILIYOIBIWA JIJINI DAR


Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Temeke, Engelbert I. Kiondo (kushoto) akiwaonesha waandishi wa habari na maofisa wa polisi shehena ya sukari iliyokamatwa.

Kamanda Kiondo akionesha sehemu walipolazwa walinzi katika ghala la Haruni Zacharia Enterprises lililopo Mbagala jijini Dar.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Temeke, Engelbert I. Kiondo (kushoto) akiwaonesha waandishi wa habari na maofisa wa polisi shehena ya sukari iliyokamatwa.
Kamanda Kiondo akionesha sehemu walipolazwa walinzi katika ghala la Haruni Zacharia Enterprises lililopo Mbagala jijini Dar.
Kamanda Kiondo akionesha geti la ghala hilo la sukari lililovunjwa na wezi.
Jeshi la polisi pamoja na waandishi wa habari wakiwa katika ghala la sukari lililovunjwa.
 Jeshi la Polisi mkoa wa Kipolisi Temeke limefanikiwa kukamata mifuko 1312 ya sukari ambapo kila mmoja una kilo 50 ambayo iliibwa katika ghala la kampuni ya Haruni Zacharia Enterprises huko Mbagala jijini Dar es Salaam. Mifuko hiyo ya sukari imekamatwa usiku wa kuamkia leo Agosti 6 mwaka huu. Kwa mujibu wa Kamanda Kiondo watuhumiwa 12 wametiwa nguvuni kwa kuhusika na wizi huo. Walinzi wanne wa ghala hilo baadhi yao wamekutwa wamejeruhiwa na wengine wakiwa wamefungwa kamba miguuni.

No comments:

Post a Comment