Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Saturday, September 14, 2013

PICHA ZA PADRI ALIYEMWAGIWA TINDIKALI AKIWA HOSPITALINI AKIPATA MATIBABU




Hali ya wasiwasi imezidi kutanda  kwa baadhi ya watu  kisiwani Zanzibar baada ya Padri Anselmo Mwangamba(pichani) wa Parokia ya Mpendae kumwagiwa tindikali na watu wasiojulikana leo majira saa 10 jioni .Padri Mwangamba ambaye ni Mkuu wa kituo cha malezi cha vijana kilichopo Cheju Mkoa wa Kusini Unguja ambacho hutunza vijana kwa ajili ya kuwapatia mafunzo mbali mbali alikumbana na mkasa huo wakati akitoka kupata huduma za mawasiliano ya mtandao katika maeneo la Mlandege. 

Taarifa toka kwa Daktari wa hospitali ya Mnazi mmoja ambaye alimpokea padri huyo Dr. Abdalla Haidari alisema  Padre huyo ameumia sehemu ya uso na kifua, inaonyesha  amejeruhiwa na maji ambayo baada ya kuyafanyia uchunguzi tumegunduwa kuwa ni tindikali . Pia mfanyakazi mmoja wa duka linalotoa huduma za mawasiliano ya mtandao aliyejitambulisha kwa jina la Salma (kwenye video) alikiri kutokea kwa tukio hilo na kukiri kuwa  huyo padre ni mteja wake na alipata huduma hapo dukani kwake.

Hilo ni tukio la tano kwa watu mbali mbali kumwagiwa tindikali huko Zanzibar,  tukio hilo limethibitishwa na Kamanda wa Polisi mkoa wa mjini Magharibi Unguja, Mkadam Khamis  na amedai uchunguzi  wa kina umeanza.

No comments:

Post a Comment