Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, October 4, 2013

82 wafariki wakijaribu kwenda Ulaya



lampedusa-rescue-unhcr_45684.jpg
Maafisa katika kisiwa kikubwa cha Sicily katika bahari ya meditarenia wanasema kuwa wamepata maiti 82 baada ya meli iliyokuwa imewabeba takriban wahamiaji 500 wa kiafrika kushika moto na kuzama katika kisiwa cha Lampedusa.
Shughuli kubwa ya uokozi inaendelea kuwatafuta manusura.
Meya wa mji huo anasema kuwa walionusurika wako hatika hali ya mshutuko na walimwambia kuwa moto mdogo uliwashwa baada ya meli kukwama na lengo lilikuwa kuitisha msaada.
Lakini alisema kuwa moto ulisambaa kupita kiasi na ikawa vigumu kuudhibiti.
Kisiwa cha Lampedusa kiko kati ya Tunisia na Sicily na kimekuwa kiingilio kikuu cha wahamiaji kuingia barani Ulaya

No comments:

Post a Comment