Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, October 3, 2013

WATANZANIA WAJITOKEZA KWA WINGI KATIKA MKUTANO WA MWIGULU NCHEMBA DMV-MAREKANI

SWAHILI TV TELEVISION YAKO YA KIZALENDO ILIKUWEPO KATIKA KUHAKIKISHA MATUKIO YOTE YANAWEKWA KATIKA KUMBUKUMBU MUHIMU ZA VONGOZI WETU
Mhe. Naibu Katibu Mkuu CCM Mwigulu Nchemba akijibu kwa ufasaha na kwa ustadi mkubwa kabisa maswali kutoka kwa wananchi waliohudhuria Mkutano wa Maendeleo ya Nchi yetu uliofanyika DMV Jumapili Sept 29,2013
Liz Haynes akifuatilia Mkutano kwa Makini
Mh. Mwigulu akifafanua jambo katika Mkutano wake na Watanzania DMV
Mhe. Naibu Katibu Mkuu CCM Mwigulu Nchemba aliruhusu kila swali liulizwe na aliyajibu yote kwa ufasaha na kwa ustadi mkubwa hakuna mwananchi aliyerudi na dukuduku nyumbani. Pichani Kulia aliyeketi ni Msaidizi wa Rais Bw. Rajab Luhwavi
Dada Georgina Lema akiuliza Maswali yake kwa hisia kali




 Mchungaji Melchizedeki Martulu kutoka kanisa la Bethel World Outreach akiuliza Maswali

 Mama Cherehani akiuliza Maswali yake bila uoga kwa ujasiri mkubwa

 Mhe. Mwigulu alikuwa na kazi kubwa ya kumjibu kila mmoja


 Miss Temeke akisikiliza kwa umakini mkubwa sambamba na wananchi wengine


 Bw. Dotto aliyekuja na Jazba nzito alipewa uhuru wa kuuliza Maswali yake yote na kuridhika

 Dotto alisikika akisema alikuwa amekuja kumtukana Mheshimiwa Nchemba, badala yake aliridhika sana na kumkubali Mhe. Mwigulu na kukiri kwamba alikuwa hamjui na sasa baada ya kumsikia anamuelewa kuwa ni  mtu safi, makini na Kiongozi bora kwa Taifa letu.


 Eliserena Kimolo naye alikuwa na maoni, maswali na hoja binafsi kwa Mgeni Rasmi

 Ofisa Ubalozi Mindi Kasiga akiwa ndani ya Mavazi ya CCM akiwa busy na simu yake wakati Mkutano wa Mhe. Naibu Katibu Mkuu CCM Mwigulu Nchemba ukiendelea
 Ofisa Ubalozi Suleiman Saleh naye alihudhuria, alimwagiwa sifa na Katibu Uenezi na Itikadi CCM kwa kuwa mstari wa mbele kuijali jamii ya kitanzania na watanzanio wote bila upendeleo.






 Hidaya Mahita naye alikuwa na machache ya kuuliza

 Bw. Mohamed Matope akiuliza maswali yake yaliyopata majibu kama wadau wengine


 

No comments:

Post a Comment