Pages
(Move to ...)
Home
IT page
Advertisement
Sports news
comedy zone
Contanct and where we are
JICHO LA CAMERA YANGU
▼
Thursday, November 28, 2013
KINANA AMALIZA ZIARA YAKE ILEJE
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kushoto akiongozana na Balozi Katiti wa shina namba moja la Kata ya Sange wilayani Ileje Mkoani Mbeya ambapo katibu mkuu huyo alizungumza na wanachama wa shina hilo na kumpongeza balozi kwa kazi nzuri ya kujitolea na kukijenga chama cha Mapinduzi, amewataka viongozi wote wa mikoa, wilaya na kata kuwatembelea mabalozi .Ili kuwapa moyo na kutambua umuhimu wa kazi zoa kwani hao ndiyo wenye wanachama lakini viongozi wa juu hawana wanachama kazi yao ni kuongoza na kuhakikisha ilani ya uchaguzi ya chama cha mapinduzi inatekelezwa kwa mafanikio ili kuwapa maendeleo wananchi, Katika ziara hiyo Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ameongozana na Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi Ndugu Nape Nnauye na Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kiamataifa.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-ILEJE – MBEYA)
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wa pili kushoto akipata maelezo ya Mkuu wa wilaya ya Ileje Rosemary Sinyamule wakati alipokagua daraja la mto Songwe katika mpaka wa Tanzania na Malawi mahali ambapo kunatakiwa kujengwa ofisi ya uhamiaji ili kurahisisha kazi za tasisi hiyo muhimu nchini, Wilaya ya Ilenje kata ya Isongole inapakana na kata na kijiji cha Mbilima wilaya ya Chitipa kwa upande wa Malawi
Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wa kata ya Kalembo kutokana na kushindwa kutembelea na kuweka shada la maua katika kaburi la marehemu Steven Kibona ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Fedha na kutumikia nchi kwa uadilifu mkubwa kwa sababu ya hali mbaya ya utelezi katika barabara kutokana na mvua iliyokuwa ikiendelea kunyesha katika kata hiyo, Kinana amesema yeye na marehemu Steven Kibona waliwahi kufanya kazi wakiwa manaibu waziri wa Ulinzi na akasifu uadilifu wa marehemu Steven Kibona kushoto ni Mke wa marehemu Mama Kibona
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wa kata ya Kalembo
Mwenyekiti wa halmashauri ya Kyela Bw. Mohamed Mwala wakati alipokuwa akitoa kero ya mbolea inayotengenezwa na kiwanda cha Minjingu ambayo inadaiwa na wakulima wa Ileje kuwa haina viwango na inasababisha mazao kuharibika.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na Mke wa Marehemu Steven Kibona Mama Kibona kwenda kupata chakula cha mchana katika kata ya Kalembo leo mchana.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na ujumbe wake wakivuka daraja wakivuka daraja la mto Songwe wakati alipokagua daraja hilo hapo wanaingia upande wa Malawi.
Kikundi cha ngoma ya asili ya watu wa Ileje kikitumbuiza kabla ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kuzungumza na wananchi katika kata ya Kalembo leo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza
Mkuu wa wilaya ya Ileje Rosemary Sinyamule wakati akitoa maelezo zaidi kuhusu uimarishaji wa miundimbinu ya Wilaya ya Ileje ili kurahisisha shughuliza kibiashara katika mpaka wa Tanzania na Malawi wakati alipokagua daraja la mto Songwe katika mpaka huo leo kulia ni
Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa
na kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya na Mbunge wa jimbo la Mbozi Mashariki Mh. Godfrey Zambi.
Kutoka kulia ni wapiganaji Richard Mwaikenda wa Jambo Leo, John Bukuku Mkurugenzi wa Mtandao wa www.fullshangweblog.com na Laude Mwambona kutoka gazeti la Mwananchi wakivinjari katika mpaka wa Malawi na Tanzania wakati Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alipokagua daraja hilo wapiganaji hao ni miongozi mwa wanahabari waliopo katika msafara huo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na ujumbe wake wakirejea upande wa Tanzania.
Maofisa wa Idara ya Uhamiaji wakiwa katika ofisi yao iliyopo Isongole inadaiwa jengo hilo ni la kupanga
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na mkuu wa kituo hicho cha idara ya uhamiaji Isongole Bw. Fredrick Luhanga wakati alipotembelea katika ofisi hiyo.
Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi Ndugu Nape Nnauye akiwa amekaa na wanachama wa CCM katika shina namba moja Kata ya Sange.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akielekea nyumbani kwa balozi
Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa Siasa na Uhusiano wa Kmataifa
na akishiriki ujenzi wa msingi wa jengo la kituo cha afya cha Lubanda
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana aki
shiriki ujenzi wa msingi wa jengo la kituo cha afya cha Lubanda leo
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ileje Bi Sylivia Siriwa
TUNAOMBACLICK HAPA LIKE PAGE YETU KWA NEWS UPDATES ZA KILA SIKU
No comments:
Post a Comment
‹
›
Home
View web version
No comments:
Post a Comment