Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, November 27, 2013

Kwanini Che Guevara Alichagua Code Name ' Tatu' ?

1465320_10201800860835986_1151306460_n_5b071.jpg
Ndugu zangu,
Nimepata kuandika juu ya kitabu nilichosoma kiitwacho " The African Dream"- The diaries of the revolutionary war in the Congo. Ama hakika ni kitabu chenye maelezo yenye kusisimua, kufurahisha na kusikitisha juu ya mwanamapinduzi Che Gueavara na harakati zake za mapambano ya ukombozi wa kimataifa.
Ni kweli kuwa Che aliingia Dar April 1965 na alikutana na Nyerere ili kupata baraka zake kabla ya kwenda Congo Mashariki.
Hata hivyo, katika kitabu hicho Che hakuweka wazi jina la hotel aliyoishi alipokuwa Dar. Lakini, kwa Dar ilivyokuwa hata miaka ya 70 ambayo nami nina kumbukumbu ya kutosha kwa kuona, basi,kulikuwa na restaurants nne pale katikati ya jiji ambazo nami nimeziona kwa macho na nimepata kuingia mara kadhaa utotoni, nazo ni Zahir Restaurant ( Sasa New Zahir Restaurant iliyo Mtaa wa Msikiti).
Ni Restaurant hii ambayo Che alikwenda mahali hapo kwa chakula na chai. Kulikuwa pia na Royal Restaurant na Nakhuda Restaurant zote zikiwa Mtaa wa Jamhuri. Restaurant ya nne iliitwa The Khalid pale mtaa wa Kipande.(P.T)
Hitimisho. Kama Che Guevara alikunywa chai na kula chakula Zahir Restaurant,basi,yawezekana kabisa kuwa ama aliishi Zahir Guest House iliyokuwa nyuma ya mgahawa huo, au kwenye Ubalozi wa Cuba pale Upanga. Taarifa za kuaminika zaidi ni kuwa Che aliishi Ubalozi wa Cuba.
Na kwanini hilo halikuwekwa wazi katika kitabu cha kumbukumbu zake siwezi kujua,maana siamini kama aliishi kwenye moja ya hoteli za gharama jijini Dar kwa vile hakutaka hata kwenda New Africa Hotel ambapo ndio ilikuwa kijiwe cha akina Abeid Karume na wapigania ukombozi wengine. Ni kwa vile, Che Guevara hakutaka kabisa kuonekana na mawakala wa CIA.
Na kwanini Che alichagua Code Name ' Tatu'? Sababu hasa haifahamiki, isipokuwa, jambo hilo liliwashangaza sana wapiganaji wa KiCongo kwenye Uwanja wa Mapambano, maana, walishangaa sana kuwa, katika mawasiliano, mwenye kuitwa TATU ndiye aliyekuwa na sauti zaidi kuliko MBILI na MOJA. MBILI ilikuwa ni Code name ya mtu wa pili na wa karibu na Che, wakati MOJA alikuwa ni mkalimani!
Maggid Mjengwa,
Iringa,




No comments:

Post a Comment