Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, November 28, 2013

MUME ADAIWA KUMUUWA MKEWE NJOMBE .


 Mwanamke Aliyeuawa Kwa Kukatwa Kichwani Njombe.

 Pichani ni Anjelika Mhenga Aliyeuawa na Mtu Anayesadikika Kuwa ni Mumewe Jana Majira ya Saa Tatu Asubuhi Mtaa wa Idundilanga Eneo la Ujamaa B Mjini Njombe.



Mtuhumiwa wa Mauaji ya Anjelika Mhenga Bwana Elia Mtweve Mkazi wa Kijiji cha Mkiu Wilayani Ludewa Aliyetoroka Baada ya Kudaiwa Kumuua Mke Wake Njombe.



Na  Gabriel  Kilamlya  Njombe

 Mtu Mmoja Mkazi wa Matembwe Wilayani Njombe Anjelika Mhenga Mwenye Umri wa Miaka 37 Amekutwa Amefariki Dunia Baada ya Kupigwa na Kitu Chenye Ncha Kali Sehemu za Kichwani na Mtu Anayesadikika Kuwa ni Mumewe Katika Eneo la Ujamaa "B" Mtaa wa Idundilanga Mjini Njombe.

Akizungumza na www.gabrielkilamlya.blogspot.com Kaka wa Marehemu Huyo Bwana Joseph Mhenga Amesema Kuwa Tukio la Mauaji ya Dada Yake Limetokea Jana Novemba 26 Mwaka Huu Majira ya Saa Tatu Asubuhi Baada ya Kupata Taarifa Kwa Njia ya Simu na Mdogo Wake Ambaye Alieleza Kuwa Naye Kapigiwa Simu na Shemeji Yake Kuwa Amegombana na Mkewe Hivyo Ameamua Kusafiri.

Aidha Bwana Mhenga Amesema Kuwa Shemeji Yake Huyo Anayedaiwa Kuhusika na 
Mauaji Hayo Anafahamika Kwa Jina la Elia Mtweve Mwenye Umri wa Miaka 41 Mkazi wa Kijiji cha Mkiu Wilayani Ludewa Ambao Wote Kwa Pamoja Walikuwa Wakiishi Njobe Kama Mume na Mke. 

Amesema Kuwa Hakuna Taarifa Zozote za Sababu za Kutokea Kwa Tukio Hilo Walizozipata Zaidi ya Taarifa za Ugomvi Waliokuwa Nao Licha Ya Kwamba Hata Ugomvi Huo Haifahamiki Ulitokana na Nani.

Kwa Upande Wake Balozi wa Eneo La Ujamaa 'B' Mtaa wa Idundilanga Bi.Catherine Nyatto Amesema Kuwa Baada ya Kupata Taarifa za Tukio Hilo Akafika na Kubaini Tukio Hilo Baada ya Kukuta Milango Yote Imefungwa Kwa Nje Ndipo Alipochukua Jukumu la Kuvunja Mlango Mmoja wa Nje na Kisha Kwenda Kutoa Taarifa Polisi.

Hata Hivyo Mwili wa Marehemu Anjelika Mhenga Umeruhusiwa Kuzikwa Leo Huko Matembwe Tarafa ya Lupembe Ambako Ndiko Nyumbani Kwao.

                      TUNAOMBA CLICK HAPA LIKE PAGE YETU KWA NEWSUPDATES ZA KILA SIKU
 
CHANZO JACKSON AUDIFACE  

No comments:

Post a Comment