Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, January 8, 2014

KISOMO CHA MAREHEMU ZAINAB BUZOHERA DMV

Rais wa Jumuiya ya Watanzania DMV Bwn. Iddi Sandaly akiongea kwenye kisomo cha mpendwa wetu Zainab Buzohera kulichofanyika jana Jumanne Jan 7, 2013 katika ukumbi wa mirage uliopo Langeley Park, Maryland na kuhudhuriwa na Watanzania wa DMV na majimbo mengine kama New York, New Jersey, Massachusetts, Georgia, Ohio, Pennsylvania na kwingineko. Mwili utaondoka leo Jumatano Jan 8, 2014 na kufika Ijumaa Dar ses Salaam, Tanzania siku ya Ijumaa na utaambatana na dada ya marehemu Jasmine Bernett na Mume wa marehemu Dullah wakiwemo Watanzania kadhaa hapa Maryland na majimbo mengine.
Mwambata wa Jeshi katika Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Canada, Colonel Adolph Mutta akiongea kwa niaba ya Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Liberata Mulamula ambaye yupo Tanzania.
Wafiwa mdogo wa marehemu Ngalu Buzohera (wapili toka kushoto baibui nyeusi) na Dada wa narehemu Jasmine Bernett (watatu toka kushoto) wakifuatilia kisomo cha mpendwa wao kilichofanyika jana Jumanne Jan 7, 2014 Langeley Park Maryland.
Juu na chini ni Jopo la Watanzania wakiwemo maafisa Ubalozi wakiongoza kisomo cha kumuombea mpendwa wao kilichofanyika jana Jumanne jan 7, 2014 Langley Park, Maryland.
Juu na chini umati wa Watanzania wa DMV na majimbo mengine waliohudhuria kisomo cha mpendwa wetu Zainab Buzohera kilichofanyika Jumanne Jan 7, 2014 Langeley Park, Maryland katika ukumbi wa Mirage.

No comments:

Post a Comment