Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, January 28, 2014

MKULIMA MKAZI WA NYAMHANGA IRINGA MJINI AKUTWA AMEJINYONGA




MKAZI  wa Nyamhanga  kata ya Kitwiru mjini  Iringa   Bw  Daud Malongo (84) aliyekuwa akijishughulisha na kilimo amekutwa amefariki dunia baada ya kujinyonga kwa kutumia kipande cha pazia.
Kamanda wa polisi mkoani Iringa Ramadhani Mungi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea mnamo tarehe 27 januari majira ya saa 9:30 jioni.
Kamanda Mungi ameuambia mtandao huu wa matukio daima kuwa marehemu alikutwa ndani ya stoo ya nyumbani kwake akiwa tayari ameshafariki huku chanzo cha tukio hilo la kusikitisha bado hakijafahamika.

 katika tukio lingine JESHI la polisi mkoani Iringa linamshikilia Isaya Kimanga (30) raia wa DRC Congo kwa kosa la kuingia Nchini bila kibali.
Kamanda Mungi alisema tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 26 januari katika Kijiji cha Mtua tarafa ya Mazombe wilaya ya Kilolo ambapo askari polisi walikuwa doria.CHANZO www.matukiodaima.com

No comments:

Post a Comment