MBUYU
Twite na Didier Kavumbagu wa Yanga wana siku 30 tu za kuitumikia klabu
hiyo kabla ya kufanya uamuzi mgumu wa kubaki au kuondoka Yanga. Siku
hizo zinaanza leo mpaka Aprili 19 msimu utakapomalizika na Aprili 20
watakapokuwa na kikao Jangwani kutathmini msimu ikiwemo kupongezana kama
watafanikiwa kutetea ubingwa wao.
Mastaa
hao ni miongoni mwa wachezaji wanane wa Simba na Yanga ambao wapo sokoni
na wanaweza kusaini mkataba na klabu yoyote muda wowote kuanzia sasa na
siku ambazo klabu zao zitawamiliki kihalali hazizidi 30 kuanzia sasa.
Ingawa
klabu zao zimekuwa bize kuwania nafasi za juu kwenye msimamo wa Ligi Kuu
Bara, baadhi ya wachezaji hao wameanza nyodo na kusisitiza kwamba
hawatasaini na klabu hizo mpaka mwisho wa msimu huku ikionekana kama
wanataka kutingisha kiberiti wapewe dau nono.
Uchunguzi
wa Mwanaspoti ambao umethibitishwa na wachezaji hao umeonyesha kwamba
wachezaji wa Yanga ambao mikataba yao inamalizika mwezi Aprili 19 Ligi
ya Bara itakapomalizika ni kipa, Ali Mustapha ‘Barthez’ ambaye habari za
uhakika zinaeleza mazungumzo yake ya kurejea Simba yanakwenda vizuri,
beki wa pembeni Mbuyu Twite, washambuliaji Didier Kavumbagu na Said
Bahanuzi aliyegoma kutolewa kwa mkopo kwenye usajili wa dirisha dogo
msimu huu.
Kwa
upande wa Simba wachezaji wanne ambao mikataba yao ipo ukingoni ni
viungo, Uhuru Selemani na Ramadhani Chombo ‘Redondo’, kipa raia wa Ghana
Yaw Berko ambao wote hata hivyo hawajawahi kuwa na uhakika wa namba
kwenye kikosi cha kwanza tangu kuanza kwa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu
Bara.Mchezaji mwingine ni beki wa pembeni Haruna Shamte.
Twite
amesisitiza kwamba hatasaini mkataba mpya na Yanga mpaka msimu
utakapomalizika huku ikitafsiriwa kwamba anataka kutingisha kiberiti ili
kurekebishiwa baadhi ya vipengele kwenye mkataba wake na amewaambia
marafiki zake wa karibu kwamba hana raha kwa jinsi anavyoishi na vigogo
wa Yanga kwa sasa.
Habari za
ndani zinadai kwamba mchezaji huyo amewahi kufanya mazungumzo na
viongozi wa Azam miezi michache iliyopita hivyo ana imani kwamba huenda
wakampa ofa.
Kavumbagu
ambaye amekuwa tegemeo kwenye fowadi ya Yanga alisema: “Bado sijasaini
mkataba mwingine wa kuichezea Yanga, mkataba wangu unamalizika mwishoni
mwa msimu huu (Aprili 19), ingawa tayari nimeanza mazungumzo ya awali
ambayo bado hatujafikia muafaka wa kusaini mkataba mpya.”
SOURCE: GAZETI LA MWANASPOTI
No comments:
Post a Comment