Maafisa wa usalama nchini Misri
wanasema afisa wa ngazi ya juu wa polisi nchini Misri ameuawa katika
shambulio la bomu katika mji mkuu Cairo.
Polisi huyo Brigedia Generali Ahmed Zaki aliuawa
katika kitongoji cha Magharibi mwa mji huo baada ya bomu lililokuwa
limetegwa chini ya gari lake kulipuka.Mjini Alexandria,afisaa mwingine mmoja aliuawa wakati wa shambulizi dhidi ya kile maafisa wanasema ni maficho ya wanamgambo.
Wapiganaji wa kiisilamu wameongeza kasi ya mashambulizi dhidi ya maafisa wa usalama na kuwaua mamia tangu jehi kumwondoa mammalakni Morsi.
Mnamo siku ya Jumapili, mtu aliyekuwa amejihami kwa bunduki alimpiga risasi na kumuua afisaa mmoja wa polisi aliyekuwa anashika doria.
Shambulizi hilo lilitokea siku moja baada ya polisi mwingine kuuawa mjini Cairo na kundi la wapiganaji wajulikanao kama Ajnad.
Kundi hilo linasema linashambulia polisi kwa sababu ya msako unaofanywa dhidi ya kundi la Muslim Brotherhood. Zaidi ya watu 1,300 wameuawa na wengine
16,000 kuzuiliwa.
Ghasia hizi huenda zikatishia usalama wakati wa uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi Mei, ambapo aliyekuwa mkuu wa majeshi Abdul Fattah al-Sisi anatarajiwa kushinda.Chanzo Bbc Swahili
No comments:
Post a Comment