Arsenal wakishangilia ushindi wao usiku huu.
WASHIKA bunduki wa London, Arsenal FC wamezidi kujihakikishia kubaki Nne Bora kwenye Ligi Kuu ya England baada ya kuibamiza bao 3-0 Newcastle usiku huu kwenye Uwanja wa Emirates jijini London.
Mabao ya Arsenal yamewekwa kimiani na Laurent Koscielny, Mesut Ozil and Olivier Giroud.
Kwa matokeo ya leo, Arsenal wamefikisha pointi 73 baada ya kucheza mechi 36 wakiwa nafasi ya nne huku anayewafuatia kwa nyuma Everton akiwa na pointi 69 baada ya mechi 36 wote wakibakiwa na mechi mbili mkononi.
No comments:
Post a Comment