SIMBA SC watakabiliana na Yanga katika mechi ya kufunga pazia la ligi kuu soka Tanzania bara jumosi ya wiki hii kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Timu hizi zitakutana zikiwa na mafanikio tofuati msimu huu ambapo Yanga wameambulia nafasi ya pili, huku Mnyama akijikongoja katika nafasi ya nne.
Simba na Yanga zinapokutana katika mechi za ligi au mashindano mengine, wachezaji, mabenchi ya ufundi, viongozi na mashabiki wa klabu hizi kongwe nchini wanakuwa katika presha kubwa.
Unapozungumzia historia ya soka la Tanzania, ni dhambi kubwa kutozitaji klabu hizi mbili zenye mashabiki kila kona ya nchi hii.
Mengi yanatokea kila mechi zao zinapokaribia. Wachezaji mara nyingi wanasakiziwa kuuza mechi pale timu moja inapofungwa.
Wakati mwingine inasemekana viongozi wa timu hizi huenda kwa waganga wa kienyeji kwenda kuroga timu pinzani.
Suala la ushirikiana linazungumzwa sana katika klabu hizi, lakini ni jambo gumu kulithibitisha kisayansi kama kweli linafanya kazi.
Simba na Yanga zinakutana jumamosi, huku Yanga wakiwazidi wenzao kwa kila kitu.
Yanga wamecheza mechi 25 sawa na Simba sc, lakini wameweza kushinda mechi 16, kutoa sare 7 na kufungwa mechi 2 tu, hivyo kufikisha pointi 55 katika nafasi ya pili.
Pia Yanga ndio klabu iliyofunga mabao mengi zaidi mpaka sasa ambapo imetikisa nyavu za timu pinzani mara 60, lakini wamefungwa mabao 18 na kuwa timu ya pili kufungwa mabao machache.
Mabingwa watetezi Azam fc wamefunga mabao 50 na kufungwa mabao 15 tu, hivyo kuwa timu yenye rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi msimu huu.
No comments:
Post a Comment