Pages

Sunday, May 11, 2014

MBEYA CITY WAPATA NAFASI YA KUSHIRIKI MASHINDANO YA CECAFA



Timu ya Mbeya City, yenye maskani yake jijini Mbeya Tanzania, imepata bahati ya kushiriki mashindano ya CECAFA Nile Basine Cup, yatakayoanza nchini Sudan May 22, mwaka huu.
Hiyo itakuwa ni bahati ya aina yake kwa timu hiyo iliyoibukia hivi karibuni na kushika nafasi ya tatu katika ligi iliyofikia ukingoni, ambapo Azam wao walifanikiwa kunyakua ubingwa wa Bara.


Akizungumza jijini Mbeya, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati, Nicolas Musonye, alisema kuwa timu hiyo itafanikiwa kushiriki mashindano hayo mwaka huu.
Alisema kuingia katika mashindano hayo kwa Mbeya City ni sehemu ya kuiweka sawa timu hiyo iliyoibukia hivi karibuni ikiwa na ndoto nyingi.
Tumepanga timu ya Mbeya City iweze kushiriki mashindano haya makubwa kwa mwaka huu, tukiamini ni sehemu ya kukuza soka la Afrika kwa ujumla wake
alisema.
Musonye leo alikuwa mjini Mbeya kwa ajili ya ukaguzi wa Uwanja wa Sokoine, uliopo hapa, ambapo alipata fursa ya kutembelea na kuzungumza na baadhi ya wadau wa mpira wa miguu.

No comments:

Post a Comment