Muda wa wagonga nyundo: Kiungo wa West Ham, Stewart Downing, kulia, akishangilia bao lake na Mark Noble baada ya kutia kambani mpira dhidi ya Tottenham Hotspur'
WEST Ham imeshinda mechi ya tatu mfululizo msimu huu baada ya kuifumua Tottenham Hospur mabao 2-0 katika mchezo wa mapema wa lgi kuu soka nchini England.
Bao la kujifunga la Harry Kane na goli la adhabu ndogo kupitia kwa Stewart Downing limetosha kumpa ushindi mnono Sam Allardyce.
Gundu kwa Spurs ilianza dakika ya 25 kipindi cha kwanza baada ya Younes Kaboul kuoneshwa kadi nyekundu.
Dakika 10 baadaye, West Ham waliandika bao baada ya Andy Carroll kupiga kichwa mpira wa kona uliochongwa na Mark Noble, lakini mpira ulitua kichwani mwa mshambuliaji wa Spurs, Harry Kane na mpira kumchengua kipa Hugo Lloris na kuzama nyavuni.
Wakiwa 10 uwanjani, Spurs walijitahidi kusaka bao la kusawazisha, lakini walivurugwa zaidi baada ya goli la pili la adhabu ndogo iliyochongwa na Sterwart Downing.
West Ham walishambulia zaidi kipindi cha pili lakini hawakuongeza bao lolote kutokana na uimara wa kipa Lloris.
Kaambulia manyoya: Hugo Lloris akishindwa kuokoa mpira wa adhabu wa Downing
Andy Carroll akiwapungia mkono mashabiki wao baada ya West Ham kuandika bao la kuongoza kutokana na Harry Kane kujifunga
No comments:
Post a Comment