Chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) kimeingiza
pikipiki 252 zitakazo tawanywa kwenye maeneo mbalimbali kwa ajili ya kuimarisha
zoezi la CHADEMA ni msingi ambalo linaendelea nchi nzima likisimamiwa na kanda
zilizoundwa mapema mwaka jana (2013), huu ni muendelezo wa kuziwezesha kanda
ziweze kuendelea kufanya kazi kwa ufanisi kwa maendeleo endelevu ya chama.
Pikipiki hizo pia zitakuwa msaada mkubwa katika kipindi hiki
ambapo chaguzi ndani ya chama zinaendelea kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini,
lakini pia ni maandalizi ya uchaguzi wa serikali za mitaa vijiji na vitongoji
unao tarajiwa kufanyika mapema mwezi Oktoba.
Lakini pia itakuwa muendelezo wa kuziimarisha kanda za
chama, kama mtakumbuka kwenye uzinduzi wa kanda kila kanda ilipatiwa gari mpya
aina ya Ford Ranger, Pikipiki mpya zenye brand ya CHADEMA M4C zaidi 126 zenye
PA system zenye uwezo wakuhutubia umati wa watu kuanzia 500 hadi 1000 na
Megaphone ndogo zaidi ya 256
Sehemu ya Shehena ya pikipi zilizowaingizwa jana
Wakati watendaji wa chama makao makuu wakiwa busy na
kushirik kupokea pikipiki hizo, jana kuna uzi uliwekwa hapa ukiwa na kichwa
"Watendaji wa CHADEMA makao makuu kugoma", na eti wanataka kumfungia
katibu mkuu Dr Slaa ofisini ili kushinikiza kuongeza mishahara; Tuliupuuza kwa
kuwa haukuwa na ukweli wowote bali ulijaa hekaya za kutunga zisizo kuwa na
msingi kwa kuwa CHADEMA kinafanya mambo yake kwa utaratibu.
Mapambano yanaendelea ili kuzidi kuwaamsha watanzania dhidi
ya ufisadi, ubadhirifu wa mali na nyara za umma na ukandamizaji wa haki za
binadamu. Mpaka kieleweke.
No comments:
Post a Comment