Pages

Wednesday, September 10, 2014

MAHAKAMA YAAMURU KABURI LA MUME KUFUKULIWA MOSHI VIJIJINI,JIONEE HAPA TUKIO ZIMA

Wachimbaji wa Kijiji cha Mandaka wilaya ya Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro wakifukua Kaburi la Marehemu Stephen Assey  kwa amri ya mahakama.
Askari Polisi wakisimamia zoezi la ufukuaji wa Kaburi hilo.


Msalaba uliokuwepo kwenye Kaburi hilo ukiwa pembeni.


Na Dixon Busagaga

Uamuzi wa kufukuliwa kwa kaburi hilo umefikiwa baada ya mke anayedaiwa kuwa ni wa ndoa wa marehemu Stephen Assey, Bi. Lucy Laurant kwenda mahakamani kuweka zuio la kuzikwa kwa marehemu katika eneo ilipo nyumba aliyokuwa akiishi na mke mdogo aliyefahamika kwa jina la Fortinata Lyimo.

 Kutokana na hali hiyo mahakama ya Hakimu mkazi Moshi iliamuru kufukuliwa kwa kaburi na mwili kuhifadhiwa hosptali hadi pale uamuzi wa mwisho utakapofanywa na mahakama hiyo. 

Globu ya Jamii kama kawaida yake itaendelea kuwapasha kila kitachojiri baada ya hatua hii ya kisheria.


CHANZO: MICHUZI BLOG

No comments:

Post a Comment