Mshambuliaji nyota wa Yanga na timu ya taifa, Taifa Stars,
Mrisho Khalfan Ngassa.
Na Richard Bukos
MSHAMBULIAJI nyota wa Yanga na timu ya taifa, Taifa Stars,
Mrisho Khalfan Ngassa, amefunguliwa kesi ya madai ya talaka namba 30/2014,
katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam na mkewe Latifa Abdul
Fundi.
Ngassa amefunguliwa kesi hiyo akidaiwa
kumtelekeza na
kumnyima matunzo ya ndoa mke wake tangu Juni mwaka 2011, migogoro ilipoanzia.
Kesi hiyo iliyoanza kuunguruma Baraza Kuu la Waislamu nchini
(Bakwata), Kitengo cha Mashauri ya Ndoa, mambo yalikwenda ndivyo sivyo kufuatia
Ngassa kutotoa ushirikiano katika baraza hilo.
Baada ya baraza hilo kushindwa kesi hiyo, liliihamishia
mahakamani hapo ambapo juzi (Jumatatu), mchezaji huyo na mkewe walitakiwa
kupanda kizimbani mbele ya hakimu waliyepangiwa, Timothy Lyon, lakini Ngassa
alishindwa kutokea kutokana na majukumu aliyokuwanayo kwenye timu ya taifa
iliyokuwa nchini Burundi.
Kufuatia udhuru huo, Hakimu Lyon aliiahirisha kesi hiyo
mpaka Septemba 30, mwaka huu ambapo Ngassa na Latifa wanatakiwa kupanda
kizimbani katika shauri hilo.
Katika kesi hiyo, Latifa anamdai, Ngassa talaka pamoja na
mgawanyo wa mali walizochuma wakiwa katika ndoa yao ikiwemo nyumba mbili, moja
iliyopo Yombo na nyingine Tegeta Basihaya jijini Dar es Salaam.
Kiwanja kimoja kilichopo Tegeta Basihaya jijini, gari aina
ya Toyota Cresta, vitanda viwili, kabati dogo la vipodozi, seti ya masofa,
meza, pasi ya umeme, majiko mawili ya kupikia, televisheni, redio kaseti,
brenda na draya.
Pamoja na mali hizo, Latifa anamdai Ngassa ampe pesa taslimu
shilingi laki mbili na nusu (250,000/) kila mwezi, tangu Juni 2011, mpaka siku
ya hukumu ambazo ni kwa ajili ya matunzo tangu alipositisha kumhudumia.
Jalada la kesi hiyo liliambatanishwa na cheti cha ndoa
kinachoonyesha wawili hao walifunga ndoa Mei Mosi, mwaka 2009, mashahidi wakiwa
Imani Madega na Saidy Rashid.
No comments:
Post a Comment