Samson Mwigamba atimuliwa uongozi ACT Tanzania ,Kitila Mkumbo apewa karipio kali
Katibu Mkuu wa ACT- Tanzania Samson Mwigamba amesimamishwa uongozi
ndani ya chama hicho kwa tuhuma za ukiukwaji wa maadili,kuvunja katiba
na ubadhirifu ndani ya chama hicho.
Taarifa kutoka ndani ya kikao cha Kamati kuu zinasema mbali na Mwigamba
pia chama hicho kimetoa karipio kali kwa viongozi waandamizi wa
chama
hicho Professor Kitila Mkumbo na Habib Mchange kwa tuhuma mbalimbali.
Ikumbukwe Samson Mwigamba,Prof Kitila Mkumbo na Zitto Kabwe walitimuliwa
uongozi ndani ya CHADEMA mapema mwaka huu kwa tuhuma kama hizi na
kusababisha kuanzisha chama cha ACT Tanzania.
Source:Mtanzania Jumatano
No comments:
Post a Comment