Pages

Thursday, December 4, 2014

TASWA WATOA MAJINA WANAOWANIA TUZO KWA MWAKA 2013/2014

Mwenyekiti Kamati ya Tuzo, Bw. Rehure Nyaulawa.

KAMATI ya Kusimamia Tuzo za Wanamichezo Bora Tanzania zinazotolewa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) ilikutana Dar es Salaam jana na kupitia majina ya wanamichezo waliopendekezwa kuwania tuzo hizo.
 Tuzo itafanyika Desemba 12 mwaka huu ukumbi wa Diamond, Jubilee (VIP), Dar es Salaam, ambapo wanamichezo mbalimbali waliofanya vizuri kati ya Juni 2013 hadi Juni 2014 watakabidhiwa tuzo zao.


Ni imani yetu kwamba zaidi ya wanamichezo 40 watakabidhiwa tuzo zao siku hiyo, ambapo kamati imejiridhisha kwamba wanaowania tuzo hiyo wanastahili kulingana na mapendekezo ya vyama vya michezo kupitia Kamati zao za Ufundi.

Mshindi wa kila tuzo ataingia katika mchakato wa kumpata Mwanamichezo Bora wa Tanzania wa mwaka 2013/2014, ambapo pia siku hiyo ya sherehe za tuzo itatangazwa zawadi ya Tuzo ya Heshima kwa yule ambaye itaonekana alikuwa na mchango mkubwa katika masuala mbalimbali ya kimichezo hapa nchini. Tuzo hizo ni kuanzia Juni 2013 hadi Juni 2014.

ORODHA KAMILI YA WANAOWANIA TUZO ZA TASWA 2013/2014

OLIMPIKI MAALUM:

Wanaume: Raphael Kalukula, Pazi Mwinyimkuu na Hatibu Matali

wanawake: Blandina Blasi, Shida Jaha na Mwanaharusi Risasi.

MPIRA WA KIKAPU;

Wanaume:Lusajo Samwel (Oilers), Erick Mchemba (ABC)

wanawake:Sajda Ahmed Lyamaiga(Don Bosco Lioness), Rehema Silomba (Don Bosco Lioness) na Orlyn Titus (Don Bosco Lioness).



MPIRA WA MAGONGO;

Wanaume:Yohana Wilson, Focus Paul, Deep Vaja

Wanawake: Valentina Quarantta, Kidawa Seremala na Mary Mhina



MPIRA WA WAVU:

Wanawake: Yasinta Remmy (Jeshi Stars), Hellena Richard (Magereza) na Teddy  Abwao (Jeshi Stars).

WanaumE: Kelvin Peter Severino (Magereza), Nassoro Sharifu (Jeshi Stars) na Athuman Rupia (Jeshi Stars).



RIADHA:

Wanawake: Zakia Mrisho, Jaqueline Sakilu na Catherine Lange

Wanaume:Alphonce Felix, Dickson Marwa na Fabian Nelson.



BAISKELI:

Wanawake:  Salome Donald, Martha Anthon na Sophia Adson.

Wanaume: Richard Laizer, Hamisi Mskala na  Gerald Konda,



GOFU:

Wanaume:Nuru Mollel, Abasi Adam na Frank Mwinuka

Wanawake: Madina Iddi, Hawa Wanyeche na Angel Eaton



GOFU YA KULIPWA:

Hassan Kadio, Yassin Salehe na Geoffrey Leverian



JUDO

Wanaume: KOMBO Masoud Amour, MBAROUK MbaroukSleiman

Wanawake: Grace Alfonce Mhanga, Salma  Omari Othman.



TENISI WALEMAVU:

Wanaume; Novatus Emmanuel Temba, Yohana  Assa Mwila, Juma Mohamed Hamisi

 Wanawake; Rehema Selemani Saidi,Bihawa Mustafa Ituji



TENISI:

Wanaume: Tumaini Martin, Emmanuel Malya na Omari Sulle

Wanawake: Rehema Athumani, Edna John, Georgina Kaindoh



NETIBOLI:

Doritha Mbunda (JKT Mbweni), Berina Kazinja (Magereza Moro), Andressa Andrea (Magereza Moro)

Ngumi za Ridhaa: Fabian Gaudence, Ahmed Furahisha na Ally Abdul Ahmed



SOKA;

Wanawake:

Sophia Mwasikili, Sherida Boniface na Amina Ally



WANAUME

Elias Maguli (Ruvu Shooting-sasa Simba), Erasto Nyoni (Azam FC) na Nadir Haroub (Yanga).



WACHEZAJI WA NJE WANAOCHEZA TANZANIA

Kipre Tchetche (Azam), Amis Tambwe (Simba) na Mbuyu Twite (Yanga).



WATANZANIA WANAOCHEZA NJE

Richard Laizer (baiskeli-Afrika Kusini/Uswisi)  

Mbwana Sammata (TP Mazembe-soka DRC), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe-soka DRC).

NGUMI KULIPWA, Francis Cheka, Ramadhani Shauri na Said Mbelwa.



MPIRA WA MIKONO

Wanaume: Hemedi Salehe (JKT), Msafiri Makoti (Ngome) na Abinery Kusena (JKT)

Wanawake: Veronica Mapunda, Subira Omary na Mwajabu Lugato



WANAMICHEZO CHIPUKIZI

Omari Sulle (tenisi)

Sheridah Boniface (soka wanawake)

Aishi Manula (soka wanaume-Azam)



MWANAMICHEZO BORA WA MWAKA 2013/2014: ATAPATIKANA MIONGONI MWA WASHINDI WA KILA KATEGORI.



TUZO YA HESHIMA:

Itatangazwa ukumbini siku ya sherehe Desemba 12 mwaka huu.



Rehure Nyaulawa

Mwenyekiti Kamati ya Tuzo


03/12/2014

No comments:

Post a Comment