Pages

Friday, December 5, 2014

Zitto: Nina sharti moja tu kurudi Chadema

Baada ya Watanzania kuliona Bunge likiwachukulia hatua vigogo waliohusika na ufisadi wa Akaunti ya Tegeta Escrow wa Sh306 bilioni, madudu mengine ya Serikali yanatarajiwa kubainika mara bada ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuanza kufuatilia sakata ya sukari nchini.
Hatua hiyo ya PAC kuanza kulifanyia kazi inatokana na malalamiko ya wamiliki wa viwanda vya sukari yanayotolewa kutokana na soko la ndani kutekwa na sukari inayoingizwa kutoka nje ya nchi na wafanyabiashara wakubwa.

Wiki iliyopita, Bunge lilifikia maazimio ya kutaka mamlaka za uteuzi ziwachukulie hatua kwa mujibu wa sheria, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa 




Sospter Muhongo na katibu mkuu wa wizara hiyo, Eliakim Maswi, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Frederick Werema kutokana na kuhusika kwao kwenye sakata la uchotwaji wa fedha hizo kwenye akaunti ya escrow na kupokea fedha hizo.

Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe anasema malalamiko na matatizo yaliyopo, watatumia kipindi cha mwezi huu na ujao kupitia suala la sukari kwa kuwa ni kubwa kuliko hata ufisadi uliojitokeza katika akaunti hiyo ya Tegeta Escrow.

“Hili suala la sukari ni kubwa kuliko hata la escrow kwani linagusa moja kwa moja maisha ya wananchi, wamiliki wa viwanda na uzalishaji na tayari tumeiita Bodi ya Sukari tujadiliane kwa kina kuhusu suala hili,” anasema Zitto.

Wamiliki wa viwanda Mkurugenzi wa viwanda vya sukari vya Kagera na Mtibwa, Seif Seif anasema hasara ambayo taifa litapata kutokana na kufungwa kwa viwanda hivyo ni kubwa kuliko serikali inavyofikiria.

Anasema jambo hilo linatokana na sukari inayozalishwa nchini- kwenye viwanda vyote vinne vya Kilombero, TPC, Kagera na Mtibwa- kuwa ni tani 320,000 huku mahitaji yakiwa ni tani 420,000.

Seif anasema kutokana na upungufu wa tani 100,000, walikubaliana na Serikali kwamba iwe inaagiza tani 100,000 ili kufidia upungufu huo, jambo ambalo linafanywa kinyume na makubaliano yao.
Dar es Salaam. Harufu ya kuisha kwa mgogoro baina ya Zitto Kabwe na chama chake cha Chadema inanukia, lakini mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini anataka kuwapo na mazungumzo kubaini tatizo ili atakayebainika kuwa alifanya makosa awe tayari kuomba radhi hadharani.
Zitto alikiri bungeni kuwa amekuwa “akimiss” harakati zilizokuwa zikifanywa na vyama vya upinzani wakati wa Bunge Maalumu la Katiba, harakati zilizozaa Umoja wa Katiba ya Wananchi na kufurahia kuhudhuria kwa mara ya kwanza vikao vya umoja huo.
Zitto, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), alipata fursa ya kuingia vikao vya Ukawa wakati wapinzani walipoungana tena kupambana dhidi ya wizi wa fedha kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow, sakata ambalo liliwekwa bayana na kamati yake baada ya Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila kulifikisha bungeni, lakini hakudokeza lolote kuhusu Chadema.
Hata hivyo, mapema wiki hii, Zitto, ambaye Novemba mwaka jana alivuliwa nyadhifa zote kwenye chama hicho kwa tuhuma za kukihujumu, lakini akafanikiwa kulinda uanachama wake baada ya kufungua kesi mahakamani na kufanikiwa kupata amri ya kuzuia asijadiliwe.
Baada ya kuongoza PAC kuchunguza wa tuhuma za Escrow na kufanikiwa kulishawishi Bunge kufikia maazimio manane ya kuwashughulikia kisheria wahusika kwenye uchotwaji huo wa fedha, kumekuwapo na wito kutoka kwa baadhi ya wafuasi wa Chadema kutaka pande hizo mbili zimalizane.
“Kabla ya jambo lolote kufanyika, ili kukata kiu ya Watanzania wanaotaka kuona tunaondoa tofauti zetu, ni lazima kusema ukweli na kila upande kuwa tayari kuomba radhi hadharani pindi ikibainika ulifanya makosa,” alisema Zitto alipotakiwa kuzungumzia harakati hizo za kumrejesha Chadema.
“Ukweli wangu ndani ya Chadema ni nini? Lakini mimi ninaona sina kosa ndani ya Chadema. Ninachotaka mimi nielezwe ukweli bila chembe ya shaka makosa yangu mimi ni nini,” alisema na kuongeza:
“Nitakuwa tayari kuomba radhi hadharani kama ikibainika nilifanya makosa na kama ikibainika chama kilifanya makosa, nacho kiwe tayari kuomba radhi hadharani na ukweli uwe mbele katika maridhiano.
“Kama hakutakuwa na ukweli itakuwa vigumu kupata mwafaka. Mimi sina tatizo. Nirudie nilivyosema bungeni kuwa nina-miss sana (ninapenda sana kuwamo kwenye) harakati za mageuzi kipindi hiki za kuiondoa CCM madarakani.”
Katika mkutano na waandishi wa habari mara baada ya kuvuliwa nyadhifa zote, Zitto alisema: “Natambua kuwa wapo ambao wangependa kutumia nafasi zao kudhoofisha mapambano ya siasa za demokrasia nchini mwetu. Napenda wanachama wa Chadema na wapenda demokrasia watambue kuwa, mimi bado ni mwanachama mwaminifu wa chama hiki.
“Kinachoendelea ndani ya chama chetu ni mapambano ya kukuza demokrasia. Ni mapambano baina ya wapenda demokrasia dhidi ya wahafidhina; waumini wa uwajibikaji dhidi ya wabadhirifu; na wapenda siasa safi dhidi ya watukuzao siasa majitaka.”
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, ambaye binafsi aliguswa na mzozo huo, hakuwa tayari kuzungumzia kumaliza matatizo baina ya chama na Zitto.
- Mwananchi

No comments:

Post a Comment