Kufuatia
matokeo ya kufungwa na watani wao wa jadi 1-0 dakika chache zilizopita,
taarifa kutoka chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya dressing room ya
Simba SC ni kwamba Haruna Moshi Boban amempiga vichwa mchezaji mwenzie
Mganda Emmanuel Okwi kwa madai ya kuikosesha ushindi timu kwa kukosa
mabao mengi ya wazi.
“Haruna
amempiga Okwi baada ya mechi kuisha huku akimtuhumu kuikosesha timu
ushindi kwa kukosa kufunga katika nafasi za wazi.Baada ya kumpiga Okwi,
Haruna ameondoka hapa uwanjani peke yake bila kuongozana na wachezaji
wenzie,” kilisema chanzo cha habari.
Mpaka sasa haijajulikana Okwi ameumia kwa kiasi gani kutokana na kipigo alichokipata kutoka kwa Boban.
No comments:
Post a Comment