Pages

Friday, October 28, 2011

Van Persie aanza mazungumzo ya mkataba

Meneja wa Arsenal Arsene Wenger ameiambia BBC kitengo cha michezo, klabu hiyo imeanza mazungumzo na Robin van Persie kuhusiana na mkataba mpya.
Robin van Persie
Robin van Persie
                   
                       
Van Persie, ambaye ni nahodha wa klabu hiyo, tayari ameshapachika mabao 13 katika mechi zote ilizocheza Arsenal msimu huu na mkataba wake wa sasa unamalizika mwezi wa Julai 2013.
Alipoulizwa moja kwa moja iwapo anafanya mazungumzo na Van Persie, Wenger alijibu: "Ndio".
"Amebakisha miezi 18 kabla ya mkataba wake wa sasa kufikia ukingoni na ninahakika atasaini mkataba mpya."
Van Persie ndiye mchezaji pekee wa Arsenal aliyebakia katika kikosi hicho ambaye aliyewahi kushinda kikombe akiichezea timu hiyo.
Meneja wa Arsenal anatarajiwa kufanya kila awezalo kumbakisha mpachika mabao wao huyo hodari baada ya kuondoka msimu huu wachezaji muhimu Samir Nasri, Cesc Fabregas na Gael Clichy.
Hata hivyo, Wenger alifanikiwa kuwachukuwa wachezaji wawili wa kiungo Yossi Benayoun na Mikel Arteta, wakati mlinzi Per Mertesacker na mshambuliaji Ju-Young Park pia waliongezwa katika kikosi cha timu hiyo.

No comments:

Post a Comment