Pages

Tuesday, May 1, 2012

RIHANNA AKWAPUA CAMERA YA PAPARAZI AKIWA UFUKWENI HUKO HAWAII.


Mwanadadiva mkali wa ngoma Cheers na nyingine kali nyingi Rihanna a.k.a Riri, akiwa ufukweni huko Hawaii katika mapumziko ya weekend Riri alijikuta akifuatiliwa na waandishi wa habari akiwa amevalia kofia ya kicowboy na bitsy bikini alimsogelea mwandishi huyo na kunyakua camera yake, rafiki yake aliyekuwa pembeni akapiga picha tukio hilo, muda mfupi Riri akatweet ili rafiki zake kwenye twitter ambao ni zaidi ya watu milioni 18 waone. Tweet yake iliandika " Me high jacking a papz" sehemu hiyo ya kunyangwa camera kwa muandishi huyo ilikuwa ni sehemu ya kuhave fun lakini waandishi ilibidi watulie tu, baada ya tukio hilo Riri aliendelea kula bata na washkaji hao. Akatweet tena " Haya sindo maisha, inakuwje kama unawafanya paparazi waingie kwenye maji na wapige picha na wewe".

Jamaa wamesahau kazi wakajichanganya na Rihanna kabla wajapeleka ofisini mzigo wafanye stories wakafanyiwa wao story, mmoja ya watu waliokuwepo eneo lile (marafiki) wakapiga picha akatengeneza businness cards yenye picha yake na Rihanna. " kuna mmoja amenipa business card yenye picha yangu na yeye.....poor dat".
Matukio kama haya sio mageni kwa Rihanna mara nyingi hua anatweet kila matukio anayoyafanya kwa hiyo journalists hakuna kazi sana ya kumfuatilia coz anatoa up date za anachokifanya mara kwa mara.Ukimfuatilia karibu anakuafanyia story hii kali sana journalists jipange mzeeiyah..

No comments:

Post a Comment