Borussia Dortmund Yaifunga mabao 2-1
Ibrahim Afellay akifanya mishe kwenye lango la Arsenal
Ajax wakishangiliak
Real Madrid nchini Ujerumani.
Katika Kundi A, Paris St Germain ilikwea nafasi ya pili kwa ushindi wa
Matokeo hayo yanaipeleka Dortmund kileleni mwa kundi mbele ya timu ya
Jose Mourinho, wakati City wanashika mkia wakiwa na pointi moja tu
baada ya kucheza mechi tatu.
Robert
Lewandowski alifunga bao dakika ya 36, kabla ya Cristiano Ronaldo
kusawazisha ndani ya dakika mbili, lakini Marcel Schmelzer akawafungia
wenyeji la ushindi dakika ya 64.
Borussia Dortmund wakishangilia kuifunga Real Madrid
Marcel Schmelzer akiifungia bao la ushindi Dormund
Olympiacos walipata ushindi wa kwanza wakitoka nyuma na kushinda 2-1
dhidi ya Montpellier nchini Ufaransa na kuongeza ugumu katika Kundi B,
baada ya Arsenal kufungwa na Schalke.
Gaetan
Charbonnier aliifungia Montpellier dakika ya 49kabla ya Vassilas
Torosidis kusawazisha dakika ya 73 na Kostas Mitroglou aliyetokea benchi
akafunga la ushindi dakika za majeruhi.
Matokeo
ya jana yanaipeleka Schalke kileleni kwa pointi zake saba, wakiizidi
moja The Gunners, na Olympiacos inakwenda nafasi ya tatu na Montpellier
inaburuza mkia.
Olympiakos wamejiweka katika nafasi nzuri
Malaga imeendeleza wimbi la ushindi kileleni mwa Kundi C baada ya kuifunga
AC Milan 1-0 na sasa inaongoza kundi hilo kwa pointi tatu zaidi. Joaquin
ndiye aliyefunga bao hilo pekee dakika ya 64 kwa pasi ya Manuel Iturra.
Mechi nyingine ya Kundi C, Zenit St Petersburg waliifunga 1-0 Anderlecht
nchini Urusi.
Alexander
Kerzhakov alifunga dakika ya 72 kwa mkwaju wa penalti, baada ya Milan
Jovanovic kuchezewa rafu kwenye eneo la hatari na Alexander Anyukov.
Katika Kundi A, Porto imeendeleza rekodi yake nzuri ya asilimia 100 kwa
ushindi wa 3-2 dhidi ya Dynamo Kiev nchini Ureno.
Wageni walisawazisha mara mbili kupitia kwa Oleg Gusev na Ideye Brown
Wageni walisawazisha mara mbili kupitia kwa Oleg Gusev na Ideye Brown
baada ya wenyeji kufunga kupitia kwa Silvestre Varela na Jackson Martinez,
kabla ya Martinez kufunga la ushindi zikiwa zimesalia dakika 12.
AC Milan walifungwa na Malaga ya Hispania
Katika Kundi A, Paris St Germain ilikwea nafasi ya pili kwa ushindi wa
mabao 2-0 dhidi ya Dinamo Zagreb nchini Croatia, Zlatan Ibrahimovic
akifunga la kwanza dakika ya 32 na Jeremy Menez akafunga la pili kabla ya mapumziko.
ARSENAL YAPIGWA VIWILI NYUMBANI LIGI YA MABINGWA
Arsene
Wenger amekula kichapo cha mabao 2-0 na timu yake ya Arsenal mbele ya
Schalke ya Ujerumani kwenye Uwanja wa nyumbani, Emirates.
TAKWIMU ZA MECHI
KIKOSI
CHA ARSENAL: Mannone, Jenkinson (Gnabry 82), Mertesacker, Vermaelen,
Andre Santos, Ramsey, Coquelin, Arteta, Podolski (Arshavin 82), Cazorla,
Gervinho (Giroud 75).
BENCHI: Shea, Koscielny, Djourou, Chamakh.
BENCHI: Shea, Koscielny, Djourou, Chamakh.
NJANO: Vermaelen, Arteta, Ramsey, Gervinho.
KIKOSI
CHA SCHALKE 04: Unnerstall, Uchida, Howedes, Matip, Fuchs, Hoger (Jones
46), Neustadter, Holtby (Barnetta 65), Afellay, Farfan, Huntelaar
(Marica 87).
BENCHI: Hildebrand, Moritz, Draxler, Kolasinac.
NJANO: Afellay, Hoger.
WAFUNGAJI WA MABAO YAKE: Huntelaar 76, Afellay 86.
MAHUDHURIO: 60,049
REFA: Jonas Eriksson (Sweden)
Klaas-Jan Huntelaar akishangilia bao la kwanza alilofunga
Huntelaar akifunga
Mikel Arteta akisikitikia kipigo
Ibrahim Afellay akiifungia la pili Schalke
Afellay akishangilia bao lake
Lukas Podolski na Marco Hoger wakigombea mpira
Afellay akilalamikia kukwatuliwa kwenye eneo la penalti, lakini akapewa njano akishutumiwa kujirusha
Francis Coquelakipambana na Marco Hoeger
Coquelin akichuana na Hoeger
Manchester United imechapwa mabao 3-1 na Ajax mjini Amsterdam katika mchezo wa Kundi D wa Ligi ya Mabingwa Ulaya
TAKWIMU ZA MECHI
VIKOSI
CHA AJAX: Vermeer, Van Rhijn, Alderweireld, Moisander, Blind, Schone
(Boerrigter 89), Poulsen, Eriksen, Sana (Enoh 74), De Jong, Babel.
BENCHI: Cillessen, Sulejmani, Veltman, Dijks, Fischer.
NJANO: Blind.
WAFUNGAJI MABAO: De Jong 45, Moisander 57, Eriksen 68.
KIKOSI
CHA MAN CITY: Hart, Richards, Kompany, Lescott (Kolarov 63), Clichy, Y
Toure, Barry (Tevez 71), Milner (Balotelli 77), Aguero, Nasri, Dzeko.
BENCHI: Pantilimon, Sinclair, Nastasic, Evans.
NJANO: Kolarov, Y Toure.
MFUNGAJI WA BAO LAO: Nasri 22.
MAHUDHURIO: 45,743.
REFA: Svein Oddvar Moen (Norway).
Christian Eriksen akishangilia bao la kwanza aliloifungia Ajax
Niklas Moisander akiifungia Ajax's bao la pili
Moisander akishangilia bao lake muhimu
Joe Hart akishuhudia nyavu zake zikitikiswa na Siem De Jong
Samir Nasri akiifungia Man City bao la kufutia machozi
Man City wanashangilia bao lao
Micah Richards akiondosha mpira hatarini
Nasri akidhibitiwa
Mario Balotelli akishuhudia kipigo benchi.. BA BIN ZUBIRY
No comments:
Post a Comment