Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Sunday, December 2, 2012

CHINA YAIVUNJA NYUMBA ILIYOKUWA KATIKATI YA BARABARA



Mafundi wakivunja Nyumba iliyokuwa katikati ya Barabara baada 
ya mmiliki wa nyumba hiyo kukubali fidia ya 260,000 yuan ($41,000) 
nyumba hiyo ilikuwa imebaki yenyewe katikati ya barabara ya  Wenling 
huko katika Jimbo la  Zhejiang na kubomolewa  Dec. 1, 2012.
 Pichani ni nyumba hiyo ambayo wameliki wake walikataa kuivunja 
wakipinga kupewa malipo kiduchu ya fidia hivyo nyumba hiyo kubaki
 peke yake na katikati ya Barabara.

Kutoka katika Kijiji cha Xiayangzhang  chifu Chen Xuecai alisema
 kwamba nyumba hiyo imevunjwa Jumamosi baada ya mmiliki 
wake mkulima Luo Baogen na mke wake, kukubali 
kupokea fidia ya yuan 260,000($41,000).

 Luo, mwenye 67, alikuwa ndio ametoka kumaliza kujenga 
nyumba yake kwa gharama ya Yuan 600,000($95,000) wakati 
serikali ilipokuja na kumuambia kuwa watamlipa fidia ya Yuan 
220,000 ($35,000) kuondoka kwenye nyumba hiyo na Bwana 
Luo akagoma malipo hayo akidai ni madogo kulinganisha na
 gharama aliyotumia kuijenga nyumba hiyo.Baadae wakapandisha
 fidia hiyo hadi Yuan 260,000($41,000) wiki iliyopita na kukubalika
 baada ya kukutana na maafisa wa Serikali.

No comments:

Post a Comment