Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, July 4, 2013

HAWA NDIO WANASOKA BORA WATANO WENYE MSHIKO MREFU ZAIDI DUNIANI

Leo nimeamua kukuletea makala hii wewe shabiki wa soka na
hata mpitiaji wa blogsite hii....Makala hii inahusu wanasoka ambao
wanavisu virefu kuliko wote duniani....
Katika safu hii nimeamua kukuletea mastaa watano
ambao kutokana na kazi ya mpira wamejitengenezea
majina na kuingiza mshiko mrefu zaidi hadi hapo walipofika....
Namba Moja ameanza Mwanasoka toka Uingereza namzungumiza
David Beckham mwenye umri wa
miaka 37 huyu ndie anaeongoza ameweka kibindoni hadi
sasa Pauni za Kiingereza 175 milioni.....!!
2.Lionel Messi Mchezaji  wa Barcelona mwenye umri
 mdogo na mwenye kasi zaidi uwanjani huyu hadi sasa
kutokana na matangazo na kazi ya mpira ameingiza kiasi
cha pauni za kiingereza
115.5 Milioni....
3.C.Ronaldo mchezaji wa Real Madrid ya Uhispania
 huyu kutokana na matangazo
na mikataba mbalimbali hadi sasa ameingiza kiasi cha 
pauni za kiingereza 112 milioni..
4.Ricardo Kaka mchezaji wa Real Madrid ndio anashikilia
nafasi hii kwa sasa kutokana na matangazo
na biashara zake binafsi ameingiza hadi sasa pauni za kiingereza 66.5 milioni
5.Ronaldinho mchezaji wa timu ya taifa ya Brazil ndio anaetufungia
 dimba akiwa ameshikilia nafasi
ya tano kwenye list hii akiwa ameingiza Pauni za kiingereza
 63milioni hadi leo kutokana na mikataba
na matangazo mbalimbali ya wahisani.....

Ni hayo tu kwa leo pitia hapa hapa kwenye blogsite yako ya kijanja
thisisdiamond.com kupata makala tofauti za watu tofauti tofauti duniani...SOURCE THISIS DIAMOND

No comments:

Post a Comment