Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, November 1, 2013

MASHABIKI wa SIMBA WAVUNJA VITI 100, ADHABU YAINYEMELEA SIMBA -

SEKUNDE chache kabla ya mwamuzi Mohamed Theofile wa Morogoro hajamaliza pambano la Ligi Kuu ya Bara kati ya Simba na Kagera Sugar, mashabiki wanaodhaniwa kuwa ni wa Simba, wamevunja viti zaidi ya 100 na kuvirusha uwanjani imefahamika.
Mwandishi wa mtandao huu alishuhudia mashabiki hao wakivunja na kuvirusha uwanjani viti hivyo baada ya mwamuzi huyo kuwapa Kagera penalti iliyofungwa na Salum Kanoni.
Mashabiki hao ambao licha ya kuwa walikaa katika majukwaa tofauti, waliweza kufanya kitendo hicho kwa kile kilichoelezwa baadaye kwamba ni kupingana na maamuzi ya mwamuzi huyo.
Viti vilivyovunjwa vingi vina rangi ya chungwa na bluu ambavyo kwa haraka haraka idadi yake inaweza kuwa zaidi ya 100.
Kutokana na hali hiyo, askari wa Jeshi la Polisi walilazimika kulipua mabomu matatu ya machozi ili kuwatuliza mashabiki hao walioonekana kuwa na hasira.
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura ameuambia mtandao huu kwamba, kwa kitendo hicho kamati ya mashindano na ile ya nidhamu zinaweza kukaa na kutathimini uhalibifu uliofanywa na mashabiki hao kisha timu husika kuwajibika kulipa.
“Kila mtu ameona kilichotokea na vurugu za kuvunja viti zilianza tangu wakati wa mapumziko hivyo uchunguzi utafanyika na klabu iliyohusika italipa faini kama utaratibu ulivyo,” alisema Wambura kwa kifupi.    
 Kipa wa akiba wa Simba, Abel Dhaila, akimlalamikia mwamuzi wa akiba baada ya mwamuzi wa kati kutoa penati katika dakika za majeruhi.
  Kipa wa akiba wa Simba, Abel Dhaila, na Kocha Mkuu, Abdallah Kibaden, wakimlalamikia mwamuzi wa akiba baada ya mwamuzi wa kati kutoa penati katika dakika za majeruhi.
 Wachezaji wa akiba wa Simba wakisikitika baada ya kuamuliwa kupigwa penati hiyo.
 Askari wakiendelea kumdhibiti shabiki aliyekamatwa baada ya mashabiki hao kuvunja viti na kuanza kuruka uwanjani.
Askari wakiendelea kudhibiti vurugu..
 Sehemu ya viti vilivyoharibiwa....

No comments:

Post a Comment