Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, November 28, 2013

NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI,PHLIPO MULUGO AFUNGUA MKUTANO WA KITAIFA WA WAKUU WA VYUO VYA UFUNDI NCHINI

001 NACTENaibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Bw.Philipo Mulugo,akifafanuliwa jambo na Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi(NACTE)Dkt.Primus Nkwera(kulia)kabla ya kufungua mkutano wa kwanza Kitaifa wa wakuu wa vyuo vya ufundi,Serikali na wadau wengine wa elimu ya ufundi,Mkutano huo wa siku tatu unafanyika  katika ukumbi wa mikutano wa Arusha (AICC) jijini Arusha.
………………………………………………………………………….
Na Mwandishi Wetu, Arusha
NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo, amesema kuanzia mwaka wa masomo 2014/15 vyuo vyote vya ufundi nchini vinaendesha mafunzo ya kozi zenye ithibati tu ili kuondoa usumbufu kwa wahitimu.
Aidha ametangaza rasmi kuanza kwa mtaala wa Stashahada ya Elimu ya Msingi ambao utaanza kutekelezwa kwa vyuo vilivyo na sifa kuanzia mwaka wa masomo wa 2014/15.
Akifungua mkutano wa kitaifa wa wakuu wa vyuo vya ufundi nchini ulioandaliwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) na kufanyika jijini hapa, atalazimika kutumia polisi kukagua na kuvifunga vyuo ambavyo wamiliki wake wanashindwa kutekeleza masharti ya vyuo vyao kupata ithibati.
“Siku hizi kumeibuka wimbi kubwa la vyuo holela vinavyoendeshwa pasipokuzingatia vigezo vilivyowekwa na NACTE.
“Jamii yetu imeendelea kuhujumiwa na watu wanaojitafutia fedha kwa njia za mkato na hasa wanaojitangaza kutoa Elimu ya Ufundi tena kwa ada ndogo,” alisema.
Aliwaasa wazazi na walezi kabla ya kuwapeleka watoto wao kujiunga na vyuo vya ufundi wahoji mambo muhimu ikiwa ni pamoja na usajili wa vyuo hivyo, taaluma za wakufunzi wake ili wawe na uhakika na taalum inayotolewa kwa watoto wao.
Aliliagiza Baraza hilo, “ikiwa katika kutekeleza agizo langu mtakutana na kikwazo cho chote basi ofisi yangu ambayo ni mamlaka ya rufaa kwa mujibu wa sheria yenu itatoa ushirikiano kuhakikisha tatizo la kozi zisizotambuliwa linadhibitiwa kwa nguvu zote.”
Alisema kabla ya kuanzishwa NACTE, serikali haikuwa na chombo mahsusi cha kuratibu elimu na mafunzo ya ufundi hali ambayo ilisababisha kila mwenye chuo kujiwekea vigezo na viwango vyake vya taaluma na hivyo kusababisha nchi kuwa na vyuo ambavyo vinatoa tuzo ambazo vigezo vyake havilingani.
“Kila mwenye chuo alikuwa akitayarisha mtaala wake wa mafunzo kama alivyoona inafaa, na hivyo, kusababisha utofauti wa viwango vya tuzo zinazotolewa baina ya chuo kimoja na kingine,” alisema.
Alisema katika mfumo wa soko huria na kutokana na kiu ya Watanzania kupata elimu ya ufundi, ilikuwa ni rahisi kudanganywa na kupewa elimu duni na pia ilikuwa vigumu kwa serikali kuweka mikakati ya kuendeleza Elimu ya Ufundi ili kukidhi mahitaji ya maendeleo ya nchi na watu wake.
Katibu Mtendaji wa NACTE, Dk. Primus Nkwera, alivitaka vyuo na taasisi za elimu za ufundi nchini zinazotoa mafunzo bila kusajiliwa pamoja na wale wote wenye nia ya kuanzisha vyuo vipya kuhakikisha vyuo vyao vinapata usajili kutoka Baraza hilo kwa mujibu wa sheria.
“Baraza linapenda kuwasisitizia wadau wote ikiwemo wazazi, wanafunzi na umma kwa uiumla kujiunga na vyuo vilivyosajiliwa na Baraza na si vinginevyo,” alisema.
Alisema matarajio ya soko la ajira ni kuona vyuo vinatoa wahitimu wenye ujuzi na maarifa yanayokidhi viwangao vya utendaji kazi katika taaluma husika.
Mwenyekiti wa NACTE Mhandisi Steven Malote, alisema baraza hilo limeweka mfumo wa tuzo za kitaifa za Elimu ya Ufundi ambazo zimeunganishwa na Tuzo za Kitaifa za Ufundi Stadi (NVA), ili kuwa na ngazi kumi za Mfumo wa Kitaifa wa Elimu ya Ufundi na Ufundi Stadi (TVET).
Pia alisema imewaka kanuni za usajili na ithibati pamoja na masharti ya vyuo/taasisi kuanzisha kozi za shahada.

No comments:

Post a Comment