Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Saturday, November 30, 2013

NAPE NNAUYE: KUHOJIWA KWA MAWAZIRI KAMATI KUU YA CCM HAKUKWEPEKI



1Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa mji wa Vwawa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika jioni ya leo katika mji huo ambao ndiyo makao makuu ya wilaya ya Mbozi, mkutano huo umehudhuriwa na wananchi mbalimbali wa mji wa vwawa, Katika ziara hiyo Kinana  ameongozana na Katibu wa NEC  Itikadi, Siasa na Uenezi Nape Nnauye na Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na Uhusiani wa Kimataifa, Akizungumza katika mkutano huo Nape Nnauye amesema Injinia Christopher Chiza Waziri wa Chakula na Ushirika aache kuzungumza na vyombo vya habari badala yake aandae majibu kwa ajili ya kuhojiwa kwenye kikao cha Kamati Kuu kwa sababu kuitwa kwake kwenye kamati kuu ya CCM hakukwepeki, Kutokana na matatizo na malalamiko ya  wakulima kuhusu pembejeo, kukopwa mazao yao na  suala zima la wakulima kuikataa mbolea ya Minjingu huku wakilazimishwa kuitumia.
1AKutoka kulia ni Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mh. Abbas Kandoro, Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana,Dr. Asha Rozi Migiro Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya na Mbunge wa jimbo la Mbozi Mashariki Mh. Godfrey Zambi na Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa Itikadi na Uenezi wakipanda miti katika eneo ambalo zahanati ya kijiji cha Mtunduru kata ya Isansa inajengwa kwa ajili ya kutunza mazingira na kuzuia upepo.PICHA NA KIKOSI KAZI CHA FULLSHANGWE-MBOZI -MBEYA3 - CopyNape Nnauye akiwahutubia wananchi wa wilaya ya Vwawa4Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa amekaa na wanachama wa CCM kijiji cha Ntunduru Kata ya Isansa5Dr. Asha Rose Migiro akiwahutubia wanambozi leo7Wapiganaji Ahmed Michuzi , Richard Mwaikenda na Bashir Nkoromo wakiwa wamepumzika kidogo8Mkuu wa mkoa wa mkoa wa Mbeya Mh. Abass Kandoro akitoka nyumbani kwa balozi katika kijiji cha Ntunduru9Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoka nyumbani kwa balozi katika kijiji cha Ntunduru10Dr. Asha Rose Migiro akitoka nyumbani kwa balozi katika kijiji cha Ntunduru12Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua ujenzi wa nyumba ya daktari katika kijiji cha Ntunduru kata ya Isansa.13Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akifurahia ngoma za asili ya wanyiha14Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimuangalia kijana Huruma Wiliam wa Kata ya Isansa wakati alipokuwa akipita kwenye kamba.16Umati wa  wananchi waliojitokeza kwenye mkutano huo.

No comments:

Post a Comment