Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, November 1, 2013

YANGA YAFANYA MAUAJI YA KUTISHA YAICHAPA JKT RUVU MABAO 4-0

 Mshambuliaji wa Yanga, aliyeingia kuchukua nafasi ya Didier Kavumbagu, Jerry Tegete, akimtoka beki wa JKT Ruvu, Nashon Naftal, wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania bara, uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Katika mchezo huo Yanga imeshinda mabao 4-0, mabao mawili yakifungwa na Mrisho Ngasa, katika dakika za 4 na 23 kipindi cha kwanza, bao la tatu limefungwa na Oscra Joshuo, katika dakika ya 50 na bao la nne limefungwa na Jerry Tegete katika dakika ya 86.
 Jerry Tegete (kushoto) akishangilia bao lake kwa staili ya kunong'oneza, huku akipongezwa na Simon Msuva (kulia) na Mrisho Ngasa.
 Didier Kavumbagu, akimfinya beki wa JKT Ruvu Mussa Zubery, wakati wa mtanange huo.
 Simon Msuva (kulia) akiruka daruga la beki wa JKT Ruvu na kuambaa na mpira, ambapo alifanikiwa kutoa pasi nzuri iliyomkuta Hamis Kiiza, aliyeshindwa kupata bao la wazi.
 Sehemu ya Jukwaa la mashabiki wa Simba, likiwa tupu, haikuweza kufahamika sababu za kutohudhuria kama ilivyokuwa katika mechi za siku za nyuma.
 Mashabiki wa Yanga, ilikuwa ni shangwe......
 Hamis Kiiza, akipiga mpira wa kichwa na kusababisha heka heka langoni mwa JKT Ruvu.
Mrisho Ngasa, akiwafinya mabeki wa JKT Ruvu.....
PICHA KWA HISANI YA SUFIANI MAFOTO

No comments:

Post a Comment